Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Rais Magufuli asifiwa

Alhamisi , 16th Nov , 2017

Naibu Waziri wa Habari Sanaa Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza amemsifu na kukiri kwamba Rais Magufuli ni kiongozi mwenye ushawishi kwa mataifa mengine ndiyo maana Mfalme wa Morrocco aliahidi kujenga uwanja wa mpira mkoani Dodoma.

Mh. Shonza ametoa sifa hizo kwa Rais Magufuli wakati akijibu swali la Mbunge wa Singida Magharibi, Elibariki Kingu ambaye aliuliza ni kwa nini serikali isiteue kati ya Mkoa wa Dodoma au Singida kuwa mji wa pili utakaoweza kuendesha mashindano ya AFCON yanayotarajiwa kufanyika nchini mwaka 2019.

Katika maswali aliyoyauliza Mh. Kingu alikuwa akitaka kujua kama tayari kuna mji wa pili umeshachaguliwa kuendesha mashindano hayo baada ya Dar es salaam kuwa wa kwanza kuteuliwa.

                                                 Mbunge wa Singida Magharibi Elibariki Kingu 

Aidha Mh. Kingu akiinadi mikoa aliyoipendekeza ameisifu kwa kusema kwamba kwa sasa Mkoa wa Singida una hoteli za kisasa za kuwamudu wageni mbalimbali pamoja na kiwanja cha mpira cha kisasa kilichikarabatiwa vizuri na Mkoa wa Dodoma ni Mkao Makuu ya nchi na kwamba Rais na viongozi wakuu pia watahamia huko.

Hata hivyo Majibu ya Serikali yaliyotolewa na Mh. Shonza ameka wazi kwamba zipo kamati zilizoundwa kufanya utafiti wa mikoa hivyo ataupendekeza mkoa wa Singida ufanyiwe utafiti kama utakidhi matakwa.

"Moja ya vigezo tunavyozingatia ni uwanja unaokidhi kiwango cha kimataifa na hoteli itakayoweza kuwa-accomodate' wageni watakaokuwepo, lakini kwa upande wa Dodoma nimpongeze Rais wetu kwa ushawishi kwa mfalme wa Morroco kujenga uwanja wa michezo Dodoma" Shonza

Ameongeza "Sisi kama wizara tutachukua mawazo yake lakini endapo uwanja wa Dodoma utakamilika kabla ya mwaka 2019 basi tutaangalia kwa namna gani uwanja huo utaweza kutumika. Tukumbuke uwanja huo unajengwa kwa hisani ya Mfalme wa Morrocco hivyo hatuwezi tukampa 'deadline'.

 

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine