Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Rais Magufuli asisitiza Serikali kuhamia Dodoma

Jumatatu , 25th Jul , 2016

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo amewaongoza watanzania katika Maadhimisho ya siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa nchini ambayo kitaifa yamefanyika katika mnara wa kumbukumbu wa mashujaa Mkoani Dodoma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli,

Maadhimisho hayo ambayo kwa mara ya kwanza yamefanyika nje ya Jiji la Dar es Salaam, mkoani Dodoma ambapo Rais Magufuli amesema hiyo ni ni moja ya harakati zake za kuhamishia serikali Mkoani Dodoma ndani ya miaka minne ya Muhula wake wa kwanza.

Akizungumza katika Maadhimisho hayo Rais Magufuli, amesema mpaka sasa Dodoma, imeshakua na miundombinu ya kutosha ya kuweza kumudu watumishi wote wa wizara zake hivyo atakafanya kila awezalo ili serikali ihamie mkoani humo haraka iwezekanavyo.

Aidha Rais Magufuli amesisitiza kauli yake ya kuwatumikia wa Watanzania bila kujali itikadi zao za vyama na kusema kila mtanzania anahitaji haki sawa na kuondokewa na kero mbalimbali zinazowafanya kushindwa kufanya maendeleo

Pia Rais Magufuli ametumia fursa hiyo kuwataka watanzania kutumia maadhimisho hayo ya siku ya Mashujaa kudumisha Amani na Umoja na kujenga uzalendo wa nchi kama walivyofanya mashujaa waliokufa katika vita kwa ajili ya kuletetea taifa.

Kwa upande wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi, amewataka Watanzania wampe ushirikiano Rais Magufuli katika dhima yake ya kuwatumikia wananchi ikiwemo kumuombea kutekeleza yale yote ambayo aliwaahidi wakati wa kampeni.

HABARI ZAIDI

Rose Senyagwa, Mchambuzi wa Masuala ya Hali ya Hewa kutoka TMA

Kimbunga "IALY" kinazidi kusogea Pwani ya bahari

Picha ya Diddy na Cassie enzi za mahusiano yake

Diddy aomba msamaha kumshambulia EX wake Cassie

Rais wa Iran Ebrahim Raisi

Rais wa Iran afariki kwa ajali ya Helikopta

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,

China yaahidi kuendelea kufadhili miradi Tanzania

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu