Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Rais Magufuli atoa neno kuhusu Hosp. ya Chato

Ijumaa , 6th Dec , 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amewataka viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato Mkoani Geita kuanza mara moja upanuzi wa majengo ya Hospitali ya Wilaya ya Chato kwa kuwa Serikali imeshatoa shilingi Bilioni 1 kwa ajili ya ujenzi huo.

Rais Magufuli.

Mhe. Rais Magufuli ambaye hakufurahishwa na taarifa za viongozi wa halmashauri hiyo kupoteza muda mwingi wakibishana juu ya upanuzi huo licha ya fedha za ujenzi kutolewa tangu mwezi Julai 2019, ameonya kuwa Serikali haiwezi kuvumilia kuona watu wakipata shida kwa uzembe wa viongozi wachache wa Halmashauri.

Amemuagiza Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Selemani Jafo na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato Bw. Eliud Mwaiteleke kuhakikisha ujenzi wa majengo hayo unafanyika na kwa gharama zinazostahili.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amemtaka Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo Dkt. Ligobeth Kalisa kuhakikisha mashine ya x-ray inafanya kazi muda wote na wananchi wanapatiwa huduma kwa wakati. Amesisitiza kuwa “sio sawa kwa Hospitali ya Wilaya kukosa huduma za x-ray, eti kwa sababu ya hakuna mikanda ya kupigia picha”.

Mhe. Rais Magufuli ametoa maagizo hayo leo tarehe 06 Desemba, 2019 aliwatembelea na kuwapa pole wagonjwa waliolazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Chato akiwemo Mzee Zephania Petro Kanoge ambaye ndiye aliyemhamasisha kuingia katika siasa mwaka 1995. 

HABARI ZAIDI

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe