Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Rais Magufuli atuma salamu kwa waziri wa ujenzi

Alhamisi , 30th Jul , 2020

Rais Dkt. John Magufuli amerejea leo Jijini Dar es Salaam akitokea Mtwara baada ya jana kuongoza mazishi ya rais mstaafu wa awamu ya tatu Hayati Benjamin William Mkapa, ambapo akiwa njiani ametoa maagizo kwa Waziri wa Ujenzi kuhakikisha barabara ya Lindi inajengwa katika maeneo yote yaliyo

Rais Dkt. John Magufuli amerejea leo Jijini Dar es Salaam akitokea Mtwara baada ya jana kuongoza mazishi ya rais mstaafu wa awamu ya tatu Hayati Benjamin William Mkapa, ambapo akiwa njiani ametoa maagizo kwa Waziri wa Ujenzi kuhakikisha barabara ya Lindi inajengwa katika maeneo yote yaliyoharibika.

Akiwa njiani rais Dkt. Magufuli amesema kuwa amelazimika kuacha kutumia usafiri wa ndege ili kuweza kutambua changamoto zinazowakabili wananchi katika mikoa ya Mtwara na Lindi ambapo amebaini kuruhusu malori yenye uzito makubwa yanayobeba mawe ya gypsum yameharibu barabara ya Nangurukuru- Lindi.

Amesema kwamba amekerwa na Wizara ya Ujenzi kwa kushindwa kuyafanyia marekebisho maeneo ya barabara yaliyoharibika na kuwahakikishia wakazi wa Somanga kuwa maeneo yote yaliyoharibika yatafanyiwa matengenezo.

“Tunatuma fedha za Bodi ya Mfuko wa Barabara (Road Fund) na tunatuma fedha za Halmashauri haiwezekani Barabara mbovu Kusini hakuna stendi Somanga, Uchaguzi unakuja, tujipange vizuri na tuchague wawakilishi ambao tutawabana na watatuwakilisha vizuri”

Aidha, Rais Dk. Magufuli amesema tayari serikali imetoa zaidi ya shilingi bilioni 20 kwa ajili ya kulipa madeni ya wakulima wa korosho na kuwaasa wananchi kuyaenzi yale mema ambayo Hayati Mkapa alifanya ikiwemo kwa kuchapa kazi kwa bidii.

“Tumeshalipa zaidi ya Tsh. Bilioni 800 kwa ajili ya korosho, tumemaliza na hii Tsh. Bilioni 20 (iliyotolewa juzi), tuendelee kushikamana na Serikali yetu na tuendelee kuchapa kazi, Mtwara na Lindi ya sasa sio kama ya kipindi cha nyuma, zinapendeza, zinafurahisha”

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava