Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Rais Morsi aanguka mahakamani na kufariki dunia

Jumatatu , 17th Jun , 2019

Rais wa zamani wa Misri, aliyetimuliwa madarakani na jeshi mwaka 2013 Mohammed Morsi, amefariki dunia ghafla akiwa mahakamani, leo Juni 17, 2019 ambapo alikuwa amehudhuria kesi yake.

Mohammed Morsi alipokuwa gerezeni.

Kwa mujibu wa runinga ya taifa ya Misri, Morsi alifika mahakamani akiwa amefunikwa kitambaa cheusi, ambapo muda mfupi baadaye alianguka na kufariki dunia hapo hapo.

Taairifa ya Television hiyo, imeeleza kuwa mwili wa Morsi umepelekwa hospitali kwaajili ya uchunguzi zaidi na baadaye kuhifadhiwa.

Mohammed Morsi alichaguliwa kuwa Rais wa kwanza wa kidemokrasia nchini Misri mwaka 2012 baada ya nchi hiyo kuongozwa kwa muda mrefu na mtawala wa zamani Hosni Mubarak aliyeondoka madarakani mwaka 2011. 

Mwaka mmoja baadaye mnamo 2013, akaondolewa madarakani kwa mapinduzi ya jeshi, kufuatia maandamano makubwa ya raia, kupinga utawala wake ambapo alifunguliwa mashtaka dhidi ya makosa ya uharifu wa kibidamu na ugaidi.

Morsi alikumiwa kifo akilaumiwa kuhusika na kutoroka kwa wafungwa wengi wakati wa mapinduzi ya mwaka 2011 nchini humo, lakini Mahakama nchini Misri ilibatilisha hukumu ya kifo mwaka 2016 hivyo rufaa yake ikaendelea kusikilizwa hadi leo kifo kilipomkuta.
 

HABARI ZAIDI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Patrobas Katambi

Wasimamizi wa uchaguzi waongezwe posho - Katambi