Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Sababu za viongozi Arusha kung'olewa zatajwa

Jumatatu , 22nd Jun , 2020

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, amezitaja sababu zilizopelekea kuwang'oa wote kwa pamoja viongozi wa Jiji la Arusha akiwemo RC, DC na DED ni kwa sababu wao walishindwa kufanya kazi kwa ushirikiano na upendo, badala yake walikuwa na malumbano yasiyo na tija.

Kushoto ni Rais John Pombe Magufuli, katikati ni aliyewahi kuwa DC Arusha Gabriel Daqarro, na kulia ni aliyewahi kuwa RC Arusha Mrisho Gambo.

Rais Magufuli ameyabainisha hayo leo Juni 22, 2020, Ikulu ya Dar es Salaam, wakati akihutubia mara baada ya kumaliza kuwaapisha viongozi aliowateua na kusema kuwa viongozi wa Arusha walishindwa kuelewana kwa kipindi cha miaka miwili, licha ya kukubali utendaji wao wa kazi lakini walimuudhi.

"Mtakumbuka hivi karibuni Arusha ilibidi nitengue uteuzi wa wote niliowateua kuanzia RC,DC na DED, kwasababu katika kipindi cha miaka miwili walikua wanagombana tu, kila mmoja ni Boss, kila mmoja anatengeneza mizengwe ya mwenzake sikufurahishwa, walifanya kazi lakini waliniudhi kutokushirikiana na kufanya yale niliyowaagiza" amesema Rais Magufuli.

Aidha Rais Magufuli amesisitiza kuwa, "Wamekaa wanabishana na kuwacheleweshea wananchi wa Arusha kupata stendi nzuri, ndiyo maana nimesema wapumzike kwanza na hili liwe fundisho kwa viongozi niliowateua, lazima mkajenge element za kuvumiliana kama unataka kubishana na kugombana nenda kabisheni nyumbani kwako na mke wako".

HABARI ZAIDI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa January Makamba

Ziara ya Rais Samia Korea kuanza rasmi Mei 31 2024

Bw. Nazar Nicholas (katikati) akikabiziwa tuzo ya WSIS 2024

Tanzania yashinda Tuzo WSIS 2024, nchini Uswisi

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20