Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Serikali kuboresha huduma kwa watalii

Ijumaa , 24th Mar , 2023

Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imejipanga kuboresha huduma kwa watalii katika nyanja mbalimbali ili kuvutia watalii wengi zaidi ikiwa ni mkakati mahsusi wa  kuwafanya watalii hao kuongeza siku  za kukaa nchini na hatimaye kukuza pato la Taifa

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mary Masanja amesema hayo katika Kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kilichofanyika leo katika ukumbi wa Utawala Annex Bungeni jijini Dodoma

Amesema moja ya mkakati wa Serikali ni kuboresha huduma za malazi kwa watalii kwa kuzirejesha hoteli za Wizara ambazo zinaendeshwa  na  Sekta Binafsi ambazo kwa ujumla wake  hazifanyi vizuri

Amefafanua kuwa na Serikali inaendelea  mikakati ya kuhakikisha hoteli hizo mara baada  kurejeshwa  zinakuwa kinara kwa kutoa huduma bora kwa watalii

Pia, amesema Serikali ina mkakati wa kuboresha maeneo ya fukwe na kuunganisha vifurushi vya safari za watalii
“Tuna mpango wa kuomba umiliki wa maeneo ya fukwe urudi Serikalini ambapo moja ya mikakati yetu kama Serikali ni  kuunganisha vifurushi vya Watalii  ili waweze kutembelea vivutio vingi zaidi katika safari zao kwa mfano wakitoka hifadhini, waende kutembelea maeneo ya malikale na wamalizie safari zao katika maeneo ya fukwe, hii itawafanya watalii waweze kuongeza siku za kukaa nchini na kuongeza mapato ya utalii” Mhe. Masanja amefafanua. 
Katika hatua nyingine, Mhe.Masanja amesema  Serikali inaendelea kutangaza vivutio mbalimbali vya utalii pamoja na  kufanya utafiti wa kujua vivutio vipi vinapendwa zaidi.

“Moja ya mkakati wa Serikali ni kufanya utafiti wa vitu ambavyo watalii wanavipenda na pia kuvitangaza vivutio vya utalii na tumejifunza kwamba watalii wengi wanapenda kupumzika katika maeneo ya fukwe baada ya kutembelea maeneo ya hifadhi , malikale na mengineyo” Mhe. Masanja amesisitiza.

Kuhusu ukarabati wa barabara kwenye maeneo ya hifadhi Mhe. Masanja amesema Serikali inaendelea kuboresha miundombinu ya barabara, viwanja vya ndege hifadhini pamoja na kuweka mazingira wezeshi ili watalii wanapofika wafurahie huduma.

Naye, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, Mhe. Timotheo Mnzava (Mb) ameishauri Serikali kuangalia namna bora ya kurahisisha mchakato wa uwekezaji wa mahoteli kwenye maeneo ya hifadhi ili kuboresha huduma za malazi kwa watalii.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Watendaji na Maafisa Waandamizi kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii na Taasisi zake.

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu