Waziri Kamwelwe ametoa kauli hiyo, leo Novemba 13, 2019, bungeni Dodoma, wakati akijibu swali kwa Mbunge wa Rombo, Joseph Selasin, ambaye alihoji juu ya kudhulumiwa kwa wananchi pindi wanapouza mazao, kutoka kwa wafanyabiashara wakigeni.
Mbunge Joseph Selasin ameuliza kuwa "jimboni Rombo tunalima Maparachichi na yananunuliwa na walanguzi kutoka Kenya, kwanini kama nchi tusinunue ndege ya mizigo ili kuwasaidia wakulima wetu kupeleka mazao nje ya nchi"
Akijibu swali hilo Waziri Kamwelwe amesema kuwa "tayari tumeshaanza kujadiliana ya namna ya kupata ndege ili kubeba mazao ya Horticultural (Matunda, Nyanya, kabeji, vitunguu, viazi), na tutaanza kwa kukodi ndege, baadaye tutanunua."