Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Serikali kushirikiana na madhehebu ya dini nchini

Ijumaa , 15th Jul , 2016

WAZIRI MKUU Kasim Majaliwa amesema Serikali itahakikisha inaunga mkono dini zote nchini na kuzipa ushirikiano wa kutosha ili ziweze kufanya kazi zake vizuri.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa

“Dini ndiyo inayojenga msingi imara kiroho, kiimani na ndiyo inajenga maadili mema. Leo tunaposema kila mtu awe muadilifu tumegundua ili tufanikiwe lazima tuweke mazingira mazuri yatakayowezesha madhehebu yote kuabudu kwa uhuru,” alisema.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo jana, wakati akizungumza kwa nyakati tofauti na wananchi wa vijiji vya Malolo na Chimbila ‘B’ akiwa katika siku ya kwanza ya ziara yake ya siku tatu ya kukagua shughuli za maendeleo wilayani Ruangwa.

Alisema Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dk. John Magufuli imegundua kuwa ili iweze kufanikiwa ni lazima ishirikian na madhehebu ya yote ili yaweze kufanya kazi zake vizuri.

“Nikiwa mtendaji mkuu wa shughuli za Serikali niliamua kuunda kamati ya amani ya Taifa ambayo inajumuisha viongozi wa dini zote. Pia nimeiagiza mikoa na wilaya zote kuunda kamati za amani ili kuhakikisha umoja na maelewano miongoni mwa dini zote nchini unakuwepo,” alisema.

Alisema lengo la kamati hizo za amani ni kuhakikisha Watanzania wote wanakuwa na maadili mema na kutambua umuhimu wa kuimarisha amani na utulivu nchini.

Akizungumzia tatizo la upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama katika vijiji vya Nanganga, Nangumbu, Mbecha, Malolo, Mpumbe na Chimbila ‘B’ alisema Serikali inalifanyia kazi suala hilo.

Alisema tayari mtaalamu wa kufanya utafiti wa maji chini ya ardhi ameshawasili katika wilaya hiyo na baada ya kukamilisha utafiti huo shughuli ya uchimbaji visima itaanza.

Waziri Mkuu alisema lengo la utafiti huo ni kutaka kubaini wingi na ubora wa maji katika eneo husika hivyo aliwataka wananchi wa eneo hilo kuwa na subira wakati suala hilo likishughulikiwa.

HABARI ZAIDI

Picha ya Diddy na Cassie enzi za mahusiano yake

Diddy aomba msamaha kumshambulia EX wake Cassie

Rais wa Iran Ebrahim Raisi

Rais wa Iran afariki kwa ajali ya Helikopta

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,

China yaahidi kuendelea kufadhili miradi Tanzania

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi