Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Serikali yafukuza wauguzi

Jumatano , 18th Apr , 2018

Serikali imewafukuza kazi wauguzi wote waliokuwa wanashiriki mgomo, baada ya kukataa kurejea kazini licha ya mwajiri wao kuridhia madai yao na kuwaongezea pesa, nchini Zimbabwe.

Katika taarifa iliyotolewa na Makamu wa Rais, Constantino Chiwenga imesema serikali imekerwa na imeona imedharauliwa kwa kiasi cha dola za Marekani 17,114,446 ambazo ni sawa na takribani 39 bilioni za Tanzania, kilichowekwa kwenye akaunti ya Wizara ya Afya ili kushughulikia malalamiko yao.

"Hii ilikuwa ishara ya nia njema ya serikali, uamuzi wa ghafla wa kuhamisha fedha katika mazingira haya magumu ya kiuchumi yanayoikabili nchi hayajaweza, kuwashawishi wauguzi kurejea kazini ili kuokoa maisha ya wagonjwa na kuwasaidia wagonjwa wanaohitaji msaada wao. Sasa inachukulia kwamba huu ni ukosefu wa huruma kwa vile wanachochewa kisiasa na pia ni kwenda kinyume cha masharti ya kazi na utumishi wa umma" amesema Makamu wa Rais Constantino Chiwenga

Tayari Rais Emmerson Mnangagwa ameidhinisha kufukuzwa kazi na kuhakikisha wauguzi wapya wenye mafunzo wanaajiriwa haraka iwezekanavyo ili waweze kuokoa maisha ya wagonjwa.

Manesi hao waliandamana kudai serikali kuwaongezea mishahara na kuboresha mazingira yao ya kazi, jambo ambalo serikali ya Zimbabwe iliamua kulitatua mara moja.

HABARI ZAIDI

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe