Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Serikali yamkingia kifua Makonda

Alhamisi , 19th Apr , 2018

Serikali kupitia Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, imesema zoezi la kuhamasisha kina mama waliotelekezwa na wazazi wenzao kwenye malezi ya watoto lililoendeshwa na mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Mkonda lipo sahihi na hajakosea.

Akijibu hoja za wabunge mbali mbali Bungeni, Waziri Ummy Mwalimu amesema zoezi hilo lilikuwa halali kwa sababu lipo chini ya kifungu cha sheria ya watoto ya mwaka 2009, ingawa kweli kulikuwa na makosa ambayo waliyafanyia kazi.

Waziri Mwalimu amesema sheria hiyo inawaruhusu maafisa wa ustawi wa jamii kusimamia suala la malezi ya mtoto pale familia inapofarakana, na Paul Makonda alipitia mgongo wa ustawi wa jamii ambayo pia ipo chini ya ofisi yake.

Zoezi lilikuwa ni halali, kwa sababu sheria ya mtoto namba 21 ya mwaka 2009, inatoa mamlaka kwa kamishna wa ustawi wa jamii kusimamia matunzo na malezi, zoezi lile liliendeshwa na maafisa wa ustawi wa jamii, suala lililojitokeza ni suala la faragha na kulinda haki za mtoto, baada ya kutoa tahadhari ile, sasa hivi zoezi linaendeshwa bila ku-expose sura za watoto, alichofanya makonda ni kuwahamasisha wanawake waende”, amesema Ummy Mwalimu.

Sambamba na hilo Waziri Ummy Mwalimu amesema wananchi wana changamoto kubwa ya kutokuwa na uelewa wa kupeleka mashtaka ya malezi ya watoto kwa ustawi wa jamii, na kuishia kubaki na mzigo wa kulea familia peke yao.

Zoezi hilo ambalo limeendeshwa na RC Makonda, limetuhumiwa kukiuka haki za mtoto, huku baadhi ya viongozi na wabunge wakilaumu na kusema kwamba suala la malezi ya mtoto ni suala la faragha na sio la kuliweka wazi kwenye jamii, huku wakitaka kiongozi huyo kuwajibishwa kwa kukiuka masuala hayo.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava