Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Sheria ya mtu binafsi kujipima VVU kupitishwa

Jumatatu , 11th Nov , 2019

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu, amesema kuwa hadi kufikia Ijumaa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania litaipitisha Sheria inayotoa mamlaka kwa mtu kujipima UKIMWI.

Waziri wa Afya Ummy Mwalimu

Hayo ameyabainisha leo Novemba 11, 2019 wakati wa ufunguzi wa semina elekezi kwa wasanii mbalimbali iliyoandaliwa na Wizara ya Afya, kwa kushirikiana na Taasisi ya Benjamin Mkapa pamoja na Baraza la watu wanaoishi na UKIMWI (NACP).

“Changamoto kubwa inayoikabili Wizara ya Afya katika suala zima la VVU na UKIMWI ni wanaume kutojitokeza kwa wingi kupima, na hapa ninavyoongea leo hadi Ijumaa sheria ya watu kujipima wenyewe Virusi vya UKIMWI majumbani kwao itapitishwa rasmi, lakini hata hivyo itampasa mtu kwenda hospitali kupima tena ili ajiridhishe hata kama atakuwa ameshajipima mwenyewe” amesema Waziri Ummy.

Waziri Ummy ameongeza kuwa Wizara yake imepeleka mapendekezo ya sheria itakayoruhusu umri wa mtu kupima Virusi vya Ukimwi uanzie miaka 15.

Aidha Waziri Ummy ametoa rai kwa wasanii wote waliohudhuria semina hiyo kutumia wafuasi wao walionao kupitia matamasha na hata mitandao ya kijamii kutoa elimu sahihi juu ya VVU na UKIMWI mwenyewe ili kutimiza lengo la Serikali la kuwa na asilimia 0 ya maambukizi mapya ifikapo mwaka 2030.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava