Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

TAKUKURU yatangaza kutaifisha mali za watu hawa

Jumanne , 26th Nov , 2019

Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Brigedia Jenerali John Mbungo, amezitaka taasisi na mashirika yote yaliyotafuna fedha za vyama vya Msingi na Ushirika kuzirudisha haraka iwezekanavyo kuanzia leo Novemba 26, na kwamba wasipofanya hivyo watafikish

Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Brigedia Jenerali John Mbungo, akikabidhiwa ripoti na Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga.

 

na kutaifishwa mali zao.

Hayo ameyabainisha wakati akipokea muhtasari wa uchambuzi wa ukaguzi wa Vyama vya Ushirika, uliofanywa na Shirika la Ukaguzi wa Vyama vya Ushirika (COASCO), kwa mwaka wa fedha wa 2018/2019, iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Wizara ya Kilimo katika mji wa Serikali ulioko Mtumba Jijini Dodoma.

"Natoa rai kwa wale wote wana Ushirika, Bodi za Ushirika na wote waliokuwa wanakusanya fedha za Saccos, waanze kurudisha fedha hizo kuanzia leo, hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao tutawachunguza na hatutaacha jiwe lolote ambalo halijageuzwa kwenye hilo suala la Ushirika" amesema Brig Jenerali Mbungo.

Aidha Jenerali Mbungo ameongeza kuwa "Ubadhirifu wowote haukubaliki kwani ni wizi kama wizi mwingine, endapo hawatarudisha sisi uchunguzi tutauanza mara moja pale ambapo kutakuwa na ushahidi hatua kali zitachukuliwa ikiwemo kupelekwa mahakamani, lakini hata kabla ya kushtakiwa kwa kushirikiana na Mwendesha Mashtaka wa Serikali tutapeleka maombi ya kutaifishwa mali walizonazo" ameongeza.

Kwa mwaka wa fedha wa 2018/2019, Serikali ilitoa maagizo kwa Shirika la COASCO kukagua Vyama vya Ushirika vyote, ambapo hadi tarehe 30 Juni, 2019 Vyama vya Ushirika vilivyosajiliwa vilikuwa 11,410, kati ya Vyama hivyo, Vyama hai ni 6,463, Vyama Sinzia ni 2,844 na Vyama ambavyo havipatikani 2,103.

Kutokana na maagizo hayo, hadi kufikia tarehe 30 Juni, 2019 COASCO ilikagua Vyama vya Ushirika vipatavyo 4,413 sawa na asilimia 102.63 ya lengo la Serikali la kukagua Vyama 4,300.

Katika vyama hivyo 4,413 vilivyokaguliwa, vyama 303 (6.87%) vilipata Hati inayoridhisha, vyama 2,378 (53.89%) vilipata Hati yenye shaka, vyama 879 (19.92%) vilipata Hati isiyoridhisha na vyama 853 (19.32%) vilipata Hati mbaya.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava