Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Uchaguzi wa marudio Zanzibar unafanyika hii leo

Jumapili , 20th Mar , 2016

Wananchi wa Zanzibar leo wanapiga kura katika uchaguzi wa marudio wa rais, madiwani na wawakilishi, uchaguzi unaofanyika baada ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar ZEC kufuta ule wa Oktoba 25 mwaka jana kwa madai ya kuwepo kwa kasoro nyingi.

Orodha ya wagombea wa nafasi ya urais kama ilivyotolewa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar - ZEC.

Mwandishi Wetu Noah Laltaika ambaye yupo Kisiwani Zanzibar kwa ajili ya kutuletea kinachoendelea katika uchaguzi huo amesema mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Dkt. Ali Mohamed Shein, amepiga kura yake katika kituo kilichopo shule ya msingi ya Bungi jimbo la Kibele mkoa wa Kusini Unguja majira ya saa moja na dakika tano mapema hii leo.

Viongozi wengine wakuu wa kitaifa wakiwemo wastaafu wamejitokea kushiriki haki yao ya kidemokrasia, kati yake yumo Makamu wa Rais Mstaafu Dkt. Mohamed Gharib Bilal, Makamu wa rais Bi. Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Pili wa Rais katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi.

Akizungumza mara baada ya kupiga yake, Dkt. Shein amesema kuwa kwa ujumla kumekuwa na hali ya utulivu visiwani humo na kwamba ni mategemeo yake hali itakuwa hivyo katika maeneo yote kwani usalama umeimarishwa.

Katika maeneo mengi kumekuwa na taarifa za idadi ndogo ya watu waliojitokeza ingawa katika vituo vingi wanawake ndio wamekuwa wengi na kuonyesha muitikio mkubwa wa kushiriki haki yao hiyo ya kidemokrasia.

Uchaguzi huo unafanyika licha ya chama kikuu cha upinzani cha Civic United Front (CUF) na vyama vingine kadhaa, kususia kwa madai ya kutotambua sababu zilizopelekea Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kufuta matokeo ya uchaguzi wa Oktoba mwaka jana.

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu