Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wabunge CHADEMA watetewa

Jumatano , 16th Mei , 2018

Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (BAVICHA), Patrick Ole Sosopi, amesema Wabunge wa CHADEMA kutolewa Bungeni sio kwasababu ya mapungufu yao bali ni uimara na uwezo wao wa kujenga hoja.

Sosopi ameyaeleza hayo leo kwenye kipindi cha KIKAANGONI kinachoruka kupitia Ukurasa wa 'Facebook' wa East Africa Television, wakati akijibu swali la mtazamaji juu ya wabunge wa chama chake kutojenga hoja na kuchangia Bungeni kama zamani.

''Tanzania kwasasa tunakumbana na tamaduni mpya ya kisiasa, kwahiyo kutoona wabunge wa CHADEMA wakichangia sio kosa lao, nimpe pole tu mtazamaji kwasababu haoni 'Bunge Live' mana halioneshwi ila wabunge wako imara'', amesema.

Mwenyekiti huyo amewatolewa mfano Mbunge wa Kibamba John Mnyika na Ester Bulaya wa Bunda, kuwa wameonesha uimara na uwezo wao ndio mana wameondolewa Bungeni hivi karibuni kwasababu watawala wanataka kusikia mazuri tu.

Sosopi ameongeza kuwa wanatamani kuona uhuru wa kufanya siasa ukiendelea kama ilivyokuwa zamani na sio kusubiri hadi wakati wa uchaguzi mwaka 2020 ndio wafanye mikutano ya kisiasa.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava