Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wafanyakazi waigomea serikali

Alhamisi , 6th Dec , 2018

Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) limepinga kanuni mpya ya kukokotoa mafao ya wastaafu iliyotolewa hivi karibuni likisema inakandamiza wafanyakazi na kusema pendekezo lao lilikuwa ni kuunganishwa kwa mifuko ya hifadhi ya jamii na si kanuni mpya ya vikokotoo inayolalamikiwa.

Pichani wafanyakazi wakiwa kwenye maandamano, lakini sio ya wakati huu.

Akizungumza na waandishi wa habari, mara baada ya kikao cha 35 cha shirikisho hilo mjini Morogoro, Rais wa TUCTA, Tumaini Nyamhokya amesema kanuni hizo ni kandamizi na zimepokewa na wafanyakazi kwa mtizamo hasi na zitashusha ari yao na ufanisi.

Kuunganishwa kwa mifuko ni hoja ya TUCTA tangu mwaka 2004 lakini kanuni mpya ni kinyume cha mapendekezo yetu. Sisi tulitaka kanuni zibaki kuwa za mwaka 2017 ambapo kikokotoo ni 1/540 na mkupuo ni asilimia 50, huku wastani wa umri wa kuishi ukiwa ni miaka 15.5", amesema Nyamhokya.

Nyamhokya amesema hoja ya ufanisi wa mifuko kwa mkupuo wa asilimia 50 hakutakuwa na shida yoyote endapo serikali italipa madeni yote ya mifuko na mifuko kuacha uwekezaji usio na tija au kuuza kabisa.

Mamlaka ya Usimamizi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) imewahi kufafanua kuhusu deni hilo ikisema serikali haijakopa katika mifuko ya hifadhi ya jamii tangu mwaka 2013 kwa sababu tayari ilifikia ukomo ambao ni asilimia 10 kwa mujibu wa mwongozo.

Kwenye vitabu vya Serikali madeni yake kwa mifuko ya hifadhi ya jamii bado yapo. Serikali haijakana madeni yake tangu kuunganisha mifuko hii na mara ya mwisho ilisema itatoa hati fungani ili kulipa hayo madeni yake", amesema Irene Isaka.

Mjadala mkubwa unaendelea nchini baada ya kutangazwa kwa kanuni mpya za sheria ya mifuko ya hifadhi ya jamii ya mwaka 2014 ambazo zinaelekeza pamoja na mambo mengine, kuwa wastaafu wote watalipwa mkupuo wa asilimia 25 ya mafao pindi wanapostaafu na asilimia 75 inayobaki watakuwa wakilipwa kama pensheni ya kila mwezi.

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA