Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

''Wahanga Karume watafutiwe eneo'' - RC Makalla

Jumapili , 16th Jan , 2022

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Amos Makalla,amewaomba wahanga wa moto Soko la Karume kuwa watulivu, kwani inaundwa kamati ya kuchunguza chanzo cha moto katika Soko la Karume ambapo vyombo vyote ya ulinzi na usalama pamoja na Afisa Biashara Jiji na mkoa wataingia kwenye kamati hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla akiwa Soko la Karume

Makalla ameyasema hayo leo Januari 16, 2022 baada ya kufika eneo la Karume Ilala Jijini Dar es salaam kujionea hali ya Soko la Karume ambalo limeteketea kwa moto alfajiri ya leo.

''Serikali itafanya jitihada ya kuhakikisha kwamba tunajua chanzo lakini pia tunakuja na suluhisho ya sisi kurejea katika kufanya biashara baada ya kupokea taarifa na maamuzi ya nini kifanyike katika soko hili,'' ameeleza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla.

''Tuwaombe muwe watulivu. Majanga haya yanapotokea yanahitaji maneno ya faraja kama ambayo tunawapa, lazima tutafute njia mbadala ili maisha yaendelee," amesema Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Amos Makalla.

''Si rahisi leo ukadhani kwamba baada ya hapa tutaacha tu kamati ifanye kazi, watu hawa walioko hapa lazima maisha yaendelee na ili maisha yaendelee ni maelekezo yangu kwamba Uongozi wa Jiji la Dar ukiongozwa na DC na Uongozi wa Soko, tuangalie namna ambavyo tunaweza kuwasaidia Wafanyabiashara hawa katika masoko ya jirani,'' ameongeza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Amos Makalla.
 

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine