Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Waliorejeshwa kutoka Afrika Kusini wahukumiwa

Ijumaa , 27th Nov , 2020

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewahukumu watu tisa kulipa faini ya Shilingi elfu hamsini (50,000), kila mmoja au kutumikia kifungo kwa miezi mitatu baada ya kukutwa na hatia ya kuondoka nchini kinyume cha sheria ya uhamiaji.

Pichani: Mfano wa pingu

Waliohukumiwa ni Shabani Saidi, Masoud Simba, Ramadhani Khamisi, Yassin Mbonde, Kioma Samuel, Chris Mrope, Michael Sempindu, Yusuf Kecha na Yasin Hamis.

Hukumu hiyo imetolewa hii leo na Hakimu Mkazi Mkuu Janeth Mtega baada ya washtakiwa hao kukiri kutenda kosa hilo.

Awali, Wakili wa Serikali Shija Sitta, aliwasomea mashtaka yanayowakabili kuwa Novemba 11, mwaka huu washtakiwa walikamatwa katika uwanja wa taifa wa Mwalimu Julius Nyerere baada ya kurudishwa kutoka nchini Afrika Kusini   na ndipo walipopelekwa katika ofisi za uhamiaji Jijini Dar es salaam kwa ajili ya mahojiano.

"Kwa kosa walilolitenda washtakiwa la kuondoka nchini bila kufuata kanuni na taratibu maalumu, naiomba Mahakama yako tukufu iwape adhabu kali ili iwe funzo kwa wengine" amesema Wakili Sitta.

Hata hivyo, kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo, washtakiwa walijitetea mbele ya Mahakama kuwa wanaomba wapunguziwe adhabu kwa sababu wamekiri kosa lao na kutorudia Tena kutenda kosa, baada ya kupewa nafasi na hakimu Mtega  ya kusema chochote.

HABARI ZAIDI

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji