Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Waliozalisha watumishi hewa kukiona

Jumatatu , 11th Apr , 2016

Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, amewataka Makatibu Tawala wa Mikoa nchini kuchukua hatua kali kwa wote waliosababisha kuwepo kwa watumishi hewa.

Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa

Amesema suala hilo la watumishi hewa limeisababishia serikali hasara kubwa hivyo ni lazima watu wote waliohusika katika mchakato huo wabainishwe na wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria za utumishi.

Waziri Mkuu Majaliwa ameyasema hayo jana, alipokuwa akipokea taarifa ya maendeleo ya mkoa wa Lindi iliyowasilisha na mkuu wa mkoa huo, Godfrey Zambi katika siku ya kwanza ya ziara yake ya kikazi wilayani Ruangwa .

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli wakati akiwaapisha wakuu wapya wa mikoa Machi 15 mwaka huu, aliwapa siku 15 kuhakikisha wanabaini watumishi hewa wote katika mikoa yao na kuwaondoa katika mfumo wa malipo.

Baada ya kufanyika kwa zoezi hilo jumla ya watumishi hewa 7,795 walibainika ambao wameisababishia serikali hasara ya sh. bilioni 7.5.

Waziri Mkuu amesema zoezi la kubaini watumishi hewa linalenga kuokoa fedha za serikali ambazo zilikuwa zinalipwa watumishi waliokufa, kustaafu wengine ni wale ambao wahusika walijiwekea majina na kisha fedha kuingia mifukoni mwa wajanja.

“Makatibu tawala wa mikoa ndio wakuu wa watumishi katika mikoa, hivyo ni lazima tusikie wamechukua hatua gani kwa wote waliosababisha kuwepo kwa watumishi hewa na si kukaa kungoja maagizo ya Rais,” alisema Mhe. Majaliwa.

Awali Mkuu wa mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi katika taarifa yake kwa Waziri Mkuu amesema mkoa huo una jumla ya wafanyakazi watoro 57 na hewa saba ambao ni marehemu, wastaafu waliokuwa wanalipwa mishahara na kuisababishia serikali hasara ya sh. milioni 36 kwa mwezi mmoja.

Amesema zoezi hilo la kubaini watumishi hewa na watoro litakuwa endelevu na wameanzisha timu kwa ajili ya kufanya uchunguzi ili kubaini sababu zilizosababisha watumishi waliokufa au kustaafu kuendelea kulipwa.

HABARI ZAIDI

Picha ya Diddy na Cassie enzi za mahusiano yake

Diddy aomba msamaha kumshambulia EX wake Cassie

Rais wa Iran Ebrahim Raisi

Rais wa Iran afariki kwa ajali ya Helikopta

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,

China yaahidi kuendelea kufadhili miradi Tanzania

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi