Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wanafunzi kupewa usafiri wao binafsi Dar

Alhamisi , 11th Oct , 2018

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda amesema serikali ya Mkoa huo ipo katika mikakati ya kuingiza magari 20 maaulum kwa ajili ya wanafunzi wa mkoa huo ili kuwaondolea adha ya usafiri na kuwapa fursa ya kuwahi masomoni hususani nyakati za asubuhi.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda akizungumza na wananchi wa Kimara.

Makonda ameyasema hayo leo alipotembelea kituo cha mabasi yaendayo haraka kilichopo Kimara, Dar es salaam, ambapo ameahidi kulitatua suala la usafiri lililojitokeza kituoni hapo sambamba na kumaliza tatizo la usafiri kwa upande wa wanafunzi wa mkoa wa Dar es salaam kwa kuwapatia magari yao binafsi.

Kuna changamoto ya wanafunzi wanapata shida ya usafiri na wengi wao ni watoto, sisi kama serikali ya Mkoa tuna mpango wa kuingiza magari 20 maalumu kwaajili ya wanafunzi wetu ili watoto hao waweze kupata fursa ya kuwahi masomoni, na mpango huo endapo wakubwa zetu wakikubali tutaanza kutumia barabara za mwendokasi”, amesema Makonda.

Aidha Makonda amewaomba wananchi wanaotumia usafiri wa mwendokasi kuipatia serikali muda wa siku tatu kulitatua tatizo la usafiri huo, ambao umekuwa kero kwa wananchi wa maeneo ya jiji la Dar es salaam huku akiagiza kufungwa kamera katika vituo vyote vya mabasi nchini kwa lengo la kuzuia uhalifu.

Tunaomba watumiaji wa usafiri huu watupatie muda wa siku tatu ili sisi pamoja na uongozi wa mabasi haya tukishirikiana na kiongozi wetu Waziri wa TAMISEMI kulitatua tatizo hili kwani yeye ndiyo atakayetoa tamko mabasi yanaongezeka lini?, utaratibu wa nauli unafanyikaje?, na lini wananchi watalipa kwa kutumia kadi ili kuziba mianya ya wizi kwenye vituo vya mabasi”, ameongeza.

Pia Makonda ametoa ruhusa kwa abiria wanaotumia usafiri huo kupiga picha ndani ya vituo vya mwendokasi huku akitoa wito kwa wananchi kuripoti vitendo vyote vya unyanyasaji vinavyofanywa na askari pamoja na wafanyakazi vituoni hapo kwa kurekodi matukio hayo kwa kutumia simu zao ili waweze kuwachukulia hatua za kisheria.

HABARI ZAIDI

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava