Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wananchi Njombe wapatiwa elimu ya Ebola majumbani

Jumatano , 5th Oct , 2022

Kufuatia Mji wa Njombe kuwa na mwingiloano mkubwa wa wageni kutoka ndani na nje ya nchi kibiashara, Serikali kupitia idara ya afya imelazimika kuchukua tahadhali madhubuti dhidi ya mlipuko wa ugonjwa wa ebola kwa kuanza kutoa elimu kwa wananchi majumbani na katika mikusanyiko

Tanzania ni mshirika wa jirani na Uganda ambayo hadi sasa imeripotiwa na mikasa ya zaidi ya 44 ya wagonjwa wa Ebola huku vifo vikifika 23 jambo linaloisukuma serikali kuanza kuchukua hatua za kujikinga.

Katika kukabiliana na tishio la ugonjwa wa Ebola, Baraza la halmashauri ya mji wa Njombe linalazimika kumwita mtaalamu wa tiba katika vikae vyake ili kuendelea kuelimisha viongozi wa siasa ili wakatumie nafasi yao kuelimisha umma juu ya ugonjwa huo.

Awali akitoa elimu kwa watumishi na viongozi wa siasa hususani madiwani Dr Isaya Mvinge ambaye ni mratibu wa tiba halmashauri ya mji wa Njombe anaeleza visababishi,dalili na namna ya kujikinga na maradhi hayo.

Wakizungumzia manufaa ya elimu walitopatiwa juu ya ugonjwa wa ebora baadhi ya madiwani akiwemo Erasto Mpete na Tumaini Mtewa wanasema imekuja katika wakati muafaka na kwamba wanakwenda kuchukua hatua ya kuelimisha umma ili kunusuru maambukizi kutoka wageni.

Katika hatua nyingine baraza la madiwani limepokea wageni kutoka serikali ya ujerumani ambao wameingia mashirikiano na halmashauri ya mji wa Njombe katika utekelezaji mradi wa utunzaji wa mazingira utakaohusisha ujenzi wa vizimba na nishati ya umeme wa upepo na elimu wenye thamani ya zaidi bil 4.Kama ambavyo Sebastian Randig mmeneja mazingira wilaya ya Miltenberg na Emmanuel George katibu tawala Njombe anavyoeleza.

HABARI ZAIDI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa January Makamba

Ziara ya Rais Samia Korea kuanza rasmi Mei 31 2024

Bw. Nazar Nicholas (katikati) akikabiziwa tuzo ya WSIS 2024

Tanzania yashinda Tuzo WSIS 2024, nchini Uswisi

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20