Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wananchi wahimizwa kupanda miti

Jumapili , 29th Jan , 2023

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mwanza, Mary Masanja amewahimiza wananchi kuwa wahifadhi wa mazingira kwa kupanda miti ili kuepukana na mabadiliko ya tabia ya nchi yanayoikumba dunia kama ukame na mafuriko

Ameyasema hayo leo katika uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Miaka 46 ya Chama cha Mapinduzi yanayotarajia kufikia kilele chake Februari 5, 2023

“Nataka niwakumbushe kwamba uhifadhi wa mazingira ni jukumu la kila mmoja wetu hivyo tuyatunze mazingira ili yaweze kututunza” amesisitiza Mhe. Masanja

Ameongeza kuwa Ujumbe wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ni kila mwananchi ahakikishe anapanda mti na kuutunza ili uweze kukua.

Amesema kufuatia  maelekezo hayo  ya Mheshimiwa Rais, Wizara ya Maliasili na Utalii imehakikisha inatumia fursa hiyo kuhamasisha wananchi kupanda miti hususan katika kipindi hiki cha mvua kwenye maeneo mbalimbali ya nchi ili kuhakikisha Tanzania inakuwa ya kijani.

Amefafanua kuwa Mheshimiwa  Rais Samia amekuwa kinara wa kuhifadhi mazingira na mwongoza njia katika uhifadhi na pia yeyendiye muasisi wa  filamu ya The  Royal tour iliyopelekea kila mtu sasa anajua masuala ya utalii na uhifadhi.

Mhe. Masanja amemshukuru Mheshimiwa Rais kwa kutoa fedha za miradi ya maendeleo katika jiji la Mwanza mathalani fedha za ujenzi wa barabara, meli, daraja la kigogo Busisi na miradi mingine ya maendeleo.

Katika hatua nyingine, Mhe. Masanja ametembelea Shule ya Sekondari Muhandu iliyopo katika Halmashauri ya jiji la Mwanza kwa lengo la kuhamasisha wanafunzi na wananchi wa eneo hilo kuwa na utamaduni wa kupanda miti.
Akiwa katika shule hiyo, Mhe. Masanja amewahimiza wananchi kuunga mkono jitihada za maendeleo zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na   Chama cha Mapinduzi ( CCM).

“CCM  ndicho chama  kinachoongoza nchi hivyo tukiunge mkono ili kuwaletea wananchi maendeleo  kwa hiyo pia tumuunge mkono Mheshimiwa Rais ili tuweze kufikisha maendeleo ya wananchi pale mlipo” amesema Mhe. Masanja.

Maadhimisho ya Miaka 46 ya Chama cha Mapinduzi yalihudhuriwa na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Taifa, Mary Chatanda ambaye alikuwa mgeni rasmi, Makamu Mwenyekiti UWT Taifa, Zainab Shomari pamoja na viongozi wengine wa UWT Taifa na wanachama wa jumuiya hiyo kutoka maeneo mbalimbali nchini Tanzania.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava