Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wanaokwamisha mapambano dawa za kulevya watajwa

Jumapili , 21st Apr , 2019

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni amemtaja Katibu wa Tume ya Dawa za Kulevya Zanzibar, Heriyangu Mgeni kuwa ni mmoja wa wanaokwamisha juhudi za serikali katika kupambana na dawa hizo nchini.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni

Akizungumza na wanahabari, April 20 viziwani Zanzibar, Naibu Waziri Masauni amesema kuwa atatoa mapendekezo kwa mamlaka inayohusika na mapambano ya dawa hizo kumwondoa katika nafasi yake kutokana na uzembe anaoufanya.

"Mimi nikiwa na dhamana, mara kadhaa nimekuwa nikimwita Katibu nikishauriana naye kwa kuwa suala la dawa za kulevya linaniumiza roho, ni mpaka leo Kisiwa cha Zanzibar chenye watu milioni 1.3 kinashindwa kupambana matatizo ya dawa za kulevya kwa kiwango kinachostahili", amesema Masauni.

"Maazimio ya kikao ilikuwa ni kushughulika na watu hao ambao Katibu alisema anawafahamu kuwa wanamkwamisha. Nilimweleza mbele ya kikao kuwa nataka unipatie data nikashughulike, naacha Bunge nakwenda Zanzibar kwa shughuli hii, siwezi kusubiri Rais John Magufuli anitumbue mimi kwasababu ya uzembe wa watu wachache", ameongeza.

Aidha Naibu Waziri huyo amesema kuwa haoni kama Zanzibar ina nia ya dhati ya kupambana na dawa za kulevya kwa aina ya Katibu huyo aliyedai anakwamisha juhudi za serikali.

Hata hivyo amegundua kuna mapungufu ya baadhi ya askari kwa kuwa wapo wanaoharibu kesi za dawa za kulevya makusudi kwa kuchukua rushwa kutoka kwa wauzaji wa dawa hizo wanaojulikana na kuwaachia mitaani na amemwelekeza Katibu wa Wizara hiyo kuunda tume maalumu itakayokuja kufanya kazi Zanzibar kuwabaini askari wanaozorotosha jambo hilo na hatua za haraka zichukuliwe.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa