Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wanne wafariki dunia baada ya kutumbukia mtoni

Jumatatu , 1st Mar , 2021

Watu wanne akiwemo Mkuu wa Chuo cha Uuguzi Lugarawa, Steven Mtega (39), wamefariki dunia kwa kuzama kwenye mto Lupali wakiwa kwenye gari waliyokuwa wakisafiria katika Kata ya Lugarawa wilayani Ludewa mkoani Njombe.

Mto

Akizungumza kwa njia ya simu Mganga Mkuu wa wilaya ya Ludewa Dkt Stanley Mlay, amesema tukio hilo limetokea Febuari 27 majira ya usiku marehemu hao walikuwa kwenye gari aina ya Toyota Harrier ambapo walikuwa Lugarawa kwenye mambo yao ya mapumziko.

"Walipata ajali kwenye mto Lupali huu mto sasa hivi una maji mengi kwa sababu ya mvua zinavyonyesha, walikuwa watu wanne kwenye mambo yao ya mapumziko Lugarawa na dereva alikuwa huyo mkuu wa chuo wakasema wabadilishe maeneo waende Mundindi sasa walivyofika maeneo hayo ndio wakaingia mtoni," ameeleza Mganga Mkuu Dkt. Mlay.

Dkt. Mlay amewataja marehemu wengine kuwa ni Marko Mpete, fundi umeme wa Lugarawa, Merk Mwalongo (35) mjasiriamali na Rukia Mfaume (28), ambaye alikuwa mhasibu wa mradi wa umeme wa Akra Lugarawa, na miili yao imehifadhiwa katika hospitali ya Lugarawa.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Lugarawa Erasto Mhagama, akizungumzia kutokea kwa tukio hilo amesema tukio hilo limetokea mpakani mwa kijiji cha Shaurimoyo na kijiji cha Amani

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava