Taarifa hiyo imetolewa leo Septemba 13 na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini na kwamba Wizara imefikia uamuzi huo ili kupisha uchunguzi wa tuhuma zinazowakabili za kukiuka Sheria za ardhi.
Miongoni mwa wafanyakazi hao waliosimamishwa kazi ni pamoja na Victor Robert Mkwavi ambaye ni Afisa Sheria Mwandamizi kutoka Makao Makuu ya Wizara, Manase Castory Nkuli ambaye ni Afisa Mipango miji Wilaya ya Sengerema pamoja na Nicodemus Hillu ambaye ni Afisa Ardhi Mkuu Wilaya ya Nkasi.
Ikumbukwe kuwa ni mwezi mmoja tu umepita, tangu Waziri Lukuvi alipowasimamisha kazi wafanyakazi wengine 183 kwa tuhuma za kuingilia mfumo wa kukadiria na kukusanya kodi ya pango la ardhi.