Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wauaji wa Wyne Lotter wazidi kuongezeka

Ijumaa , 23rd Feb , 2018

Watu watano akiwamo raia wa Burundi wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka ya kula njama ya kufanya mauaji ya mwanaharakati wa kutetea wanyama pori Wyne Lotter.

Wakili wa Serikali Mwandamizi,Yamiko Mlekano amewataja washtakiwa hao kuwa ni raia wa Burundi, Nduimana Jonas maarufu Mchungaji mkazi wa Kamenge Burundi na mfanyabiashara Godfrey Salamba mkazi wa Kinondoni Msisiri A. Wengine ni mfanyabiashara Inocent Kimaro  mkazi wa Temeke Mikoroshini, mfanyabiashara Chambie Ally mkazi wa Kia/Boma na Ofisa wa NBC, Robert Mwaipyana mkazi wa Temeke Mikoroshini. 

Washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka mawili ambapo katika shtaka la kwanza wanadaiwa kuwa walikula njama ya kufanya mauaji ya Lotter. Na katika shtaka la pili, washtakiwa hao wanakabiliwa na shtaka la mauaji ambapo wanadaiwa kutenda kosa hilo Agosti 16, 2017 katika makutano ya barabara za Chole na Haile Selasie Kinondoni Dar es Salaam kwa kumuua Lotter. 

Washtakiwa hawakuruhusiwa kujibu lolote kutokana na mahakam hiyo kutokuwa na mamlaka ya kuisikiliza kesi hiyo ambayo pia imetajwa kuwa haina dhamana. 

Washtakiwa hao, Machi 6,2018 wataunganishwa na washtakiwa watatu waliokuwa wanakabiliwa na kesi hiyo awali ambapo kesi yao ipo katika hatua ya kutajwa kwa sababu upelelezi wake bado haujakamilika, akiwemo Meneja wa Benki ya Backlays, Khalid Mwinyi mkazi wa Mikocheni B, mfanyabiashara Rahma Almas mkazi wa Mbagala B na Mohammed Maganga (61) mchimba makaburi. 

Kesi imeahirishwa hadi Machi 6, 2018 kwa ajili ya kutajwa ili kuangalia kama upelelezi utakuwa umekamilika ama la.

Wyne Lotter alikuwa Mkurugenzi na Mwanzilishi-Mwenza wa shirika lisilo la kiserikali la Palms Foundation ambalo linafanya shughuli zake nchini Tanzania kwa kupinga ujangili.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto