Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Waziri Kabudi apingwa hadharani, makundi yaungana

Jumanne , 5th Mar , 2019

Baada ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof Palamagamba Kabudi kuwataka Watanzania kuwa wazalendo na nchi yao na kutoisema vibaya au kuidhihaki, amekosolewa na makundi mbalimbali ya kijamii wakisema serikali itaendelea kusemwa vibaya na siyo nchi.

Waziri wa Mambo ya Nje, Prof. Kabudi

Baada ya kauli hiyo, mjadala mzito umezuka kwa viongozi na watu mbalimbali katika mtandao wa Twitter wakidai kwamba katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali haijatajwa kama ni nchi.

Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe amesema kwamba yeye ataendele kusema mabaya ya serikali ya nchi yake popote na wakati wowote.

"Ninaipenda sana nchi yangu Tanzania. Nimeitumikia kwa weledi kila nipatapo nafasi ya kufanya hivyo. Nimeilinda nchi yangu dhidi ya majaribu mbali mbali. Nitaisema vibaya Serikali ya Nchi yangu popote na wakati wowote inapofanya Mambo kinyume ya misingi ya katiba ya Tanzania," Zitto Kabwe.

Rapa wa muziki wa Bongo Fleva, Webiro Wasira "Wakazi' amesema kwamba Wanaoisema nchi siyo watanzania lakini kwa upande wake atazidi kuikosoa serikali pale inapoenda tofauti.

"Professor PK anafahamu hili, na inathibitishwa kwa matamshi yake na msisitizo wake. Anajaribu sana, maskini. Wanaoweza kuisema nchi yetu sio sisi, labda ungewa address kwa English. Ila mimi nitaendelea kuisema Serikali ikizingua kama kawaida," Wakazi.

Mwanasheria Jebra Kambole amesema kwamba,  "tofautisha nchi na serikali!! Nchi hatutaisema vibaya maana nchi ni wananchi, tutaitetea Daima!!! Lakini tutaisema na kuibagaza kadili Mungu atakavyotupa uhai!!!. Yani tutaibagaza serikali aseeeeeee!".

Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu amesema kwamba  Profesa Kabudi  ajulishwe kwamba hawatanyamazishwa na uovu wao, au vitisho vyao, au  ulaghai na propaganda zao, au na hongo na rushwa zao.

"Mwambieni Profesa Kabudi kwamba tutaendelea kuyasema hadharani, popote pale, ndani na nje ya Tanzania, maovu ya Serikali yetu, na ya vyombo vyake, na ya viongozi wake na ya watendaji wake", amesema Lissu.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava