Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wenye kumbi za starehe waanza kubanwa koo

Jumapili , 22nd Jul , 2018

Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imewaagiza viongozi wa Mkoa wa Mara na Wilaya ya Musoma kuchunguza tuhuma zinazohusisha kumbi za starehe wilayani humo kuruhusu watoto walio chini ya miaka 18 kuingia na kutumia vilevi ndani ya kumbi hizo.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile ametoa agizo hilo alipotembelea Mkoa wa Mara katika ziara ya kikazi ambapo alipokea malalamiko kutoka kwa wananchi kuhusu kuwepo kwa kumbi za starehe zinazowaruhusu watoto walio chini ya umri wa miaka 18 na kutumia pombe wakiwa ndani ya kumbi hizo.

Dkt. Ndugulile amesema kwamba wamiliki wa kumbi hizo wanakiuka sheria ya mtoto, hivyo wanapaswa kuchukuliwa hatua za kisheria mapema iwezekanavyo ili kuwalinda watoto hato chini ya umri wa miaka 18.

Aidha kwa mujibu wa wa kifungu cha 17 cha Sheria ya Mtoto ya mwaka 2009 kinasema mtu ambaye ni mmiliki au anayeendesha au ni msimamizi wa ukumbi wa muziki, 'Bar', au klabu ya usiku hatamruhusu mtoto kuingia katika maeneno yao.

Katika kifungu imeelezwa  kuwa "mtu atakayekiuka kifungu hiki atakuwa ametenda kosa na atakapotiwa hatiani atalipa faini ya kiasi kisichopungua Shilingi millioni moja na kisichozidi Sh millioni tano au kifungo kisichozidi miezi 12 au vyote kwa pamoja".

Baada ya agizo hilo kutoka wizarani, Mkuu wa Mkoa wa Mara, Bw. Adam Malima amesema ataendelea kuwachukulia hatua wale wote wanaofanya vitendo hivyo pamoja na kupambana na vitendo vya ukatili wa kijinsia, ndoa na mimba za Utotoni ambazo zinashamiri katika mkoa huo.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto