Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Zalisheni kwa wingi ili kuiteka SADC-Ole Nasha

Jumatano , 27th Jul , 2016

Serikali imeiagiza bodi ya machinjio ya kisasa iliyopo Kizota katika Manispaa ya Dodoma kuanza kufanya biashara ya nyama ili kuweza kuteka soko la nchi za jumuiya ya maendeleo ya kusini mwa Afrika (SADC) zinazokabiliwa na ukame.

Naibu waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, William Ole Nasha,

Naibu waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, William Ole Nasha, ametoa agizo hilo leo mjini Dodoma alipofanya ziara kwenye machinjio hayo ili kuona utendaji kazi wake katika katika kuhakikisha kuwa inakabiliana na ongezeko la watu hasa katika kipindi hiki ambacho serikali inahamia Dodoma.

Amesema machinjio hiyo sasa ianze kufanya biashara ya nyama na kuachana na kutegemea mifugo inayoletwa na wadau na wafanyabiashara ambao mara nyingi wanaleta mifugo ambayo haina ubora.

Ameongeza kuwa nchi zote za Jumuiya ya SADC zinakabiliwa na ukame mkubwa hali inayofanya hata wanyama kufa kwa kukosa malisho hivyo kuwa na uhitaji mkubwa wa nyama.

“Nchi zote 12 za SADC zina uhaba mkubwa wa nyama kutokana na kukumbwa ukame uliosababisha kukosekana kwa malisho ya wanyama na hivyo kusababisha wanyama kufa… hivyo hiyo ni fursa kwenu ninyi kuwekeza soko lenu la nyama katika nchi hizo,” alisema Olenasha.

Kwa upande wake Kaimu meneja mkuu wa machinjio hayo, Nashoni Kalinga, amesema kuwa machinjio hayo yana uwezo wa kuchinja jumla ya mbuzi na kondoo 120 kwa siku na jumla ya ng’ombe 80 huku soko kubwa likiwa ni ndani ya mkoa wa Dodoma na nchi za Kiarabu.

Alisema sehemu kubwa ya nyama ya ng’ombe inauzwa mkoani Dodoma huku nyama ya mbuzi na ile ya kondoo zikiwa na soko kubwa kwenye nchi za kiarabu kwa kuwa nyama hizo ni za kienyeji na siyo za kisasa..

Ametaja nchi ambazo nyama ya Tanzania ina soko kubwa kuwa ni pamoja na Qatar, Oman, Dubai pamoja na Kuweit.. Ametaja nchi nyingine kuwa ni Comoro na China.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa