Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Zumaridi hana kesi ya kujibu - Mahakama

Jumanne , 6th Dec , 2022

Kesi namba 12 ya mwaka 2022  inayomkabili Diana Bundala maarufu kama Zumaridi na wafuasi wake 84 ya kufanya mkusanyiko usio halali leo hii mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Mwanza imesema Zumaridi na wafuasi wake 80 hawana kesi ya kujibu huku wafuasi watatu wakikutwa na kesi ya kujibu

Akisoma maamuzi hayo Hakimu mkazi Clescensia Mushi amesema mahakama imejiridhisha pasina shaka kuwa washtakiwa walioachiwa hawakuguswa na vipengele muhimu vinavyotakiwa katika kuthibitisha makosa ya jinai kwa mujibu wa sheria.

Hakimu Clescensia amewataja washitakiwa watatu waliopatikana na kesi ya kujibu kuwa ni Juma Hamisi ambae ni mshitakiwa namba 5, Meshak Joseph mshtakiwa namba 33 na Daud Manyanda mshtakiwa namba 45

Amesema washitakiwa hao ndio pekee waliotajwa na mashahidi wa Jamhuri kuwa ndio waliosababisha majeraha na maumivu makali dhidi ya askari waliokwenda nyumbani kwa mfalme Zumaridi kuwakamata Februari 23 mwaka huu.

Amesema maamuzi hayo ya kuwaachia washtakiwa 81 yametokana na upande wa Jamhuri kushindwa kujenga kesi yao yaani "Premafacie" kwani mashahidi wake  walishindwa kutambua washitakiwa kuwa walitenda makosa au la.
Baada ya maamuzi hayo hakimu Mushi akaiahirisha kesi hiyo hadi Decemba 20, mwaka huu itakapokuja kwa kwa ajili ya utetezi kwa washitakiwa watatu waliopatikana na kesi ya kujibu.

Katika hatua nyingine kesi namba 10/2022 ya kuwazuia maafisa wa serikali kutekeleza majukumu yao inayomkabili Zumaridi na wenzake nane imeendelea leo huku upande wa Utetezi ukileta mashahidi wawili kwa lengo la kutoa utetezi wao.

Mashahidi hao wametoa utetezi wao leo mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Monica Ndyekobora na kuiambia mahakama kuwa waliwaona Askari polisi nyumbani kwa Zumaridi wakivunja mageti na kupiga mabomu ya machozi na kufikishwa polisi na baadae mahakamani.

Baada ya kusikiliza ushahidi huo Hakimu Ndyekora akaiahirisha kesi hiyo hadi kesho Desemba 7 mwaka huu atakapoendelea kusikiliza ushahidi kwa mashahidi wawili waliobaki.

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu