Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Heshima ya Bongo Fleva Dudubaya anena

Ijumaa , 23rd Jun , 2017

Mkongwe Dudubaya 'Mamba' amewaomba wakongwe wenzake kutowa -diss wasanii wadogo wanaofanya vizuri kwenye game ya sasa , huku akiongeza kama wanahitaji heshima zaidi wanapaswa kujijengea kwanza kabla ya kupatiwa.

Dudubaya akiwa na Professional Dj wa EA radio, Dj Dea ndani ya studio za EA radio.

Dudubaya amefunguka hayo leo kwenye uzinduzi rasmi wa heshima ya bongo fleva ndani ya kipindi cha Planet Bongo na kusema kwamba wasanii wakongwe wanapaswa kujitengenezea brand yao ili waweze kuendelea kuwepo kwenye 'game' huku akiongeza kwamba kama kazi zikifanyika vizuri wanaweza kurudi katika nafasi zao

"Mi ningeomba wasanii wakongwe tuache kuwa-diss hawa watoto wanaofanya vizuri katika game, cha kwanza tutambue siyo lazima kila siku tuonekane sisi tu, ndio maana tunapata watoto wa kuturithi. Lakini utakuta baadhi ya wasanii wakongwe wamekaa pamoja wanakula bangi hata sabini wanalalamikia watoto wanaojitafutia rizki zao, nawaambia mtakufa" , Dudubaya alifunguka.

Kuhusu tamasha la Heshima ya Bongo Fleva

Kipindi cha Planet Bongo chini ya East Africa radio inarudisha heshima kwa wasanii wa bongo Fleva kwa kuandaa tamasha lenye kuhusisha wasanii waliofanya kazi ya muziki miaka ya nyuma kufanikiwa  kuwaamisha watu wengi kwamba muziki ni kazi na siyo uhuni siku ya jumamosi ya julai 1 Dar Live Mbagala.

Tamasha hilo lililopewa jina la Heshima ya Bongo Fleva na kipindi cha planet bongo  litawaweka wasanii wakongwe kibao jukwaa moja ikiwa ni pamoja na kuwakutanisha na mashabiki zao huku muziki na hadithi zote zikiwa ni za zamani ili.

Baadhi ya wasanii watakaokuwepo kwenye orodha ya kupatiwa heshima hiyo ni Mkongwe Dudubaya, Mnyama TID, Z. Anton, Juma Nature, Mabaga Fresh, Mandojo na Domokaya, Solid Ground Family na wengine wengi watapigiwa mizinga ya heshima kwa kutengeneza misingi imara ya muziki.

Heshima ya Bongo fleva itatambua michango mbalimbali iliyofanywa na wasanii hao kwa Kiingilio cha shilingi 7000 za kitanzania huku wimbo ukiimbwa mmoja tu kwamba HESHIMA YA BONGO FLEVA , HIVI NDIO INAFAA KUFANYWA.

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu