Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

'Iga Tena' siyo dongo kwa mtu yeyote - Msaga Sumu

Jumamosi , 22nd Oct , 2016

Mkali wa muziki wa uswazi, anayejiita 'Mfalme wa Uswahili' Msaga Sumu amesema ngoma yake mpya aliyoipa jina la 'Iga Tena' siyo dongo kwa mtu yeyote, bali ni ujumbe wa kawaida unaotokana na maisha kila siku ya watanzania.

Msaga Sumu, akiwa ndani ya FNL

Msaga Sumu ambaye amejitambulisha katika game kupitia muziki wa singeli ametoa ufafanuzi huo wakati akiitambulisha rasmi video ya wimbo huo, kupitia kipindi cha FNL, cha EATV, na kuongeza kuwa huo ni ujumbe kwa watu wote ambao wamekuwa na kawaida ya "kukopi" vitu vya watu bila kuumiza vichwa wala kutambua kazi ya muanzilishi.

Akizungumzia video hiyo, Msaga Sumu amesema ameamua kuwa serious katika muziki na ndiyo maana amefanya kitu kikubwa zaidi katika video hiyo ambayo ameonesha mazingira halisi ya uswahilini.

Kuhusu yeye kufunikwa na baadhi ya wasanii wa singeli walioshika chati hivi sasa, Msaga Sumu ameendelea kusisitiza kuwa yeye ndiye baba wa muziki wa singeli na hakuna mtu atakayeweza kumfunika.

Amesema ameitoa mbali singeli tangu enzi za vigodoro kiasi cha kutishiwa kupelekwa mahakamani na baadhi ya wasanii wa taarab, kwa madai kuwa alikuwa akitumia muziki wao, na kuingiza sauti yake.

"Mimi ndiye mwanzilishi wa singeli, nimeipigania sana toka enzi za vigodoro kabla havijapigwa marufuku, nilikuwa na loop beat za taarabu hadi akina Mzee Yusuph wanataka kunishtaki, nimepigana hadi leo hii imefikia hapa" Amesema Msaga Sumu.

Katika hatua nyingine amedai kuwa yeye ndiye aliyekiibua kipaji cha Shlo Mwamba kwa kumpa nafasi katika kazi zake

"Nilikuwa nikipata kazi nashirikisha wanagu kibao ili nao waonekane, nakumbuka kwa mara ya kwanza mimi ndiye nimemtambulisha Sholo mwamba, nilikuwa na kazi fulani, nikampigia simu, akaja, nikampa nafasi akashika kipaza akafanya mambo, na watu wakaanza kumjua"

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava