Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Jux na Wolper wanogesha tamasha la mavazi Tanzania

Alhamisi , 3rd Oct , 2019

Wikiendi iliyopita kulifanyika maonyesho ya pili ya mavazi "Tanzania Fashion Festival" ambayo hukutanisha watanamindo na wabunifu wa mavazi kuonyesha bidhaa zao, ambapo safari hii lilihudhuriwa na mastaa kama Jux na Jacqueline Wolper.

Juma Jux akiperforme kwenye tamasha hilo

Licha ya kufanyika tamasha hilo pia walikuwa wanasheherekea mavazi ya majira ya joto , kukutanisha wapenzi wa muziki wa Jazz, vyakula , vinywaji pamoja na mtoko wa kifamilia ambao hukutanisha watu mbalimbali.

Muandaji wa onyesho hilo la ambaye ni mtangazaji wa kipindi cha NIRVANA cha East Africa Television, Deogratius Kithama amesema, nia ya tamasha hilo ni kuleta pamoja wapenzi wa mitindo na wanaopenda 'lifestyle' kwa ujumla na kutoa wabunifu wa mavazi kutokea Tanzania.

"Tumekuwa na bahati sana kwa sababu mwaka huu tumeona mabadiliko na maendeleo makubwa katika tamasha hili ukianzia maandalizi, mahudhurio ya watu na  hali hii inaonyesha kiasi gani tasnia ya mitindo inakuwa kila siku" ameeleza.

Akizungumzia uwepo wa ushindani wa mavazi waliyoonyesha kati ya Juma Jux na Jacqueline Wolper kwenye tamasha hilo Deogratius Kithama amesema,

"Wote wana "style" mbili tofauti ila nilinivutiwa na Jux alivyobadilisha bidhaa zake ambapo ameleta usasa mpya kwa kuongeza vitu mbalimbali kwa dizaini tofauti. Aidha kwa upande wa Wolper  wote tunamfahamu ni Mama wa maigizo alienda hadi Dubai kufanya manunuzi ili kuleta "material" ya kuonyesha katika tamasha hili"  ameongeza.

Pia amemaliza kwa kusema wote walitumia nguvu , gharama , muda na ubunifu katika onyesho hilo la mavazi "Tanzania Fashion Festival", ili kuhakikisha linakuwa la tofauti na matamasha mengine kwani ndio ilikuwa shauku yao.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava