Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Maneno ya kwanza ya muigizaji Lulu

Ijumaa , 16th Nov , 2018

Msanii wa filamu nchini aliyekuwa akikabiliwa na kesi ya kuua bila kukusudia, Elizabeth Michael (Lulu) amefunguka kwa mara ya kwanza baada ya kuachiwa huru Novemba 12.

Msanii Elizabeth Michael (Lulu).

Kupitia ukurasa wake wa 'Instagram' Lulu ametoa shukurani kwa kila aliyeshiriki kumuombea na kumshika mkono kwa namna yoyote ile katika kipindi chake chote cha kesi yake.

Lulu ameandika, "Kwa dhati kabisa nichukue nafasi hii kumshukuru kila aliyeshiriki kuniombea katika kipindi kigumu sana kwangu, kwa familia yangu na watu wangu wa karibu, mliolia na kusali pamoja na mimi ni wengi mno, ninaowajua na nisiowajua".

Ameongeza kuwa, "Kilikuwa kipindi chenye maumivu, matusi, dharau, hukumu za wanadamu, maneno ya kulaaniwa, majina yasiyofaa na mambo mengi ya aina hiyo, lakini nashukuru Mungu sikuyapokea kama yalivyo bali niliyapokea kama shule au somo lililojaa utukufu wake".

Lulu ameendelea kwa kusema kuwa kile kilikuwa ni kikombe na ilikuwa ni lazima akinywe, yalikuwa majira ambayo ni lazima ilikuwa apitie na mwisho yakawa mapenzi ya Mungu na yametimizwa.

Lulu alikuwa akitumikia kifungo cha miaka miwili jela, baada ya Novemba 13, mwaka jana kuhukumiwa na mahakama kuu baada ya kupatikana na hatia ya kumuua bila kukusudia aliyekuwa gwiji wa filamu, Steven Kanumba.

Hata hivyo, Aprili 26 mwaka huu, msanii huyo alibadilishiwa adhabu hiyo na kuwa ya kifungo cha nje. Kutokana na hilo, alipangiwa kazi ya kufanya usafi katika Wizara ya Mambo ya Ndani iliyopo maeneo ya Posta Jijini Dar es salaam aliyoianza tangu Mei 14 mwaka huu. 
 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava