Msanii wa BongoFleva Makamua
Akizungumza na mtangazaji JR Junior msanii Makamua amesema chanzo cha kifo mama yake ni matatizo ya Moyo na umauti ulimkuta baada ya kudondoka ghafla.
"Mama alikuwa na imani sana ya dini, kuna muda alikua akifanyiwa maombi basi anaamini Mungu atamponya na imani yake ilipelekea akaacha kutumia dawa za kutuliza presha jambo lililopelekea moyo wake ukawa unaongezeka ukubwa kila kukicha"
Aidha Makamua ameongeza kusema "Umauti umemkuta baada ya kudondoka ghafla na alipopelekwa hospitali madaktari waliamuru afanyiwe operationbaada ya vipimo, lakini walipomueka kwenye mashine ya kupumulia ubongo wake ulisoma sifuri kitu kilichoashiria alikua ameshafariki kabla ya kupatiwa huduma"