Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Msimuhusishe mama Steve- Barnaba

Jumatano , 15th Aug , 2018

Mwalimu na mwanamuziki wa bongo Fleva, Barnaba Elias 'Barnaba Classic' amedai sio kweli wimbo wake mpya wa 'tuachane mdogo mdogo', ulikuwa unamlenga aliyekuwa mpenzi wake na mzazi mwenzake Zuu Namela bali anachokifahamu yeye kuwa amewaimbia watanzania waliompa dhamana ya kuimba.

Msanii Barnaba akiwa katika picha ya pamoja na aliyekuwa mpenzi wake Zuu Namela.

Barnaba amebainisha hayo leo Agosti 15, 2018 wakati alipokuwa anazungumza na www.eatv.tv ikiwa imepita siku chache tokea alipoachia wimbo wake huo, ambao tungo zake zimeonekana kwa namna moja ama nyingine zikimlenga mama Steve na kuibua mjadala mzito kwa mashabiki zake, kuwa akili yake bado ina muwaza mpenzi wake huyo licha ya kuwa wameachana muda.

"Siwezi kuzungumzia masuala ya mzazi mwenzangu. Mmeshawahi kuona wapi mtu anamuimbia wimbo mtu mmoja kila siku, mimi nawaimbia watanzania. Watu walianza kumjua Barnaba kabla ya kuingia kwenye mahusiano. Sijaanza kuimba mapenzi leo, nafanya kazi kwaajili ya watanzania ambao wamenipa dhamana ya mimi kuwepo hapa nilipo", amesema Barnaba.

Mbali na hilo, pia Barnaba amesema yupo mbioni kuachia albamu yake tatu aliyoipa jina la 'gold' huku akiwarusha dongo wasanii wenzake, waliokuwa wanalalamika kwamba albamu hailipi na kudai wao wenyewe ndio walikosea kwa kutoa albamu nyepesi nyepesi.

"Albamu yangu ya gold itaingia sokoni rasmi tarehe 31 mwezi huu na itakuwa na jumla ya nyimbo 25 kati ya hizo, tano zimeshasikika hewani. Nimeamua kuja na albamu kwasasabu ninaamini watanzania wanapenda na kuhitaji muziki mzuri. Hatuwezi kuliacha soko la albamu kwa kuhofia kuibiwa, wizi upo duniani kote", amesisitiza Barnaba.

Albamu hiyo kwa mara ya kwanza ilipangwa kutoka mwezi Februari 2018 lakini ikahairishwa hadi Juli 2018, kutokana na kile kilichoelezwa na Barnaba kuwa wadhamini wake wakuu watatu, walipendelea hivyo ambapo pia haikufanyika na badala yake kutoka rasmi Agosti 31 mwaka huu.

Gold itakuwa albamu ya tatu kwa Barnaba ambapo ya kwanza alitoa kwenye miaka ya 2009 kuelekea 2019 iliyojulikana kwa jina la njia panda na albamu yake ya pili aliiachia mnamo mwaka 2011 kuelekea 2012 iliyoitwa kisa changu.
 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava