Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Nam-miss sana Zuu"- Barnaba

Jumatano , 13th Sep , 2017

Mwalimu na mwanamuziki wa bongo Fleva, Barnaba Elias 'Barnaba Classic' amefunguka na kudai anam-miss sana mama Steve 'Zuu Namela' japokuwa kwa sasa hayupo tayari kumrudia mzazi mwenzake huyo.

Msanii Barnaba akiwa na mama Steve 'Zuu Namela' enzi hizo mapenzi yakiwa moto moto kabla ya kuachana kwao.

Barnaba ameeleza hayo baada ya kupita muda mrefu tokea aachane na mzazi mwenzake huyo na kupelekea kuwa single mpaka kipindi hiki.

"Sitaweza kurudiana na mama watoto wangu japo nam-miss sana", amesema Barnaba.

Aidha, Barnaba amesema kwa upande wake mapenzi hayajawahi kumuendesha hata kidogo kama baadhi ya watu wengine wanavyokuwa baada ya kuachana na wapenzi wao kwa kushindwa hata kuendelea kufanya kazi zao.

"Niwe mkweli tu, mimi sijawahi kuendeshwa na mapenzi au mahusiano. Mapenzi hayana nafasi kubwa katika maisha yangu japokuwa yana nguvu kwa mtu yeyote yule, mapenzi hayajawahi kuchukua asilimia kubwa ya maisha yangu, kuniathiri wala kunitikisa", amesema Barnaba.

Pamoja na hayo, Barnaba ameendelea kwa kusema "Kila unachokiona kinatokea katika maisha yako kiwe kizuri au kibaya ni mapito tu, kwa sababu kilichotuleta duniani ni kingine na tunachokifanya ni kingine kwa hiyo muda mwingine kutendwa na vitu vingine ni kutenda dhambi zaidi 'so sometimes' unatakiwa upokee kwa furaha chochote utakachokumbana nacho katika maisha yako, kwa sababu hujui mpango wa Mungu ukoje. Ninachoamini mimi ni kwamba nilikuwa napita kwenye daraja ili niweze kuendela na safari aliyopanga Mungu 'so' sijui 'next' nilichopangiwa na Mwenyezi Mungu", amesisitiza Barnaba.

Kwa upande mwingine, Barnaba japo wameachana na Zuu lakini bado wanamawasiliano mazuri baina yao na kudai hivi karibuni aliongea naye kuulizia maendeleo ya Steve ya kimasomo na kumtumia pesa kwa ajili ya matumizi ya shule.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava