Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

The WD, vinara Dance 100% 2015

Jumatatu , 12th Oct , 2015

Kundi la kudansi la The WD watangazwa rasmi kuwa mabingwa wa mashindano ya Dance 100% 2015 baada ya kujivunia alama za kutosha na kujinyakulia zawadi ya ushindi shilingi milioni 5 sambamba na kombe kama ishara ya taji hilo.

Kundi la kudansi la The WD watangazwa rasmi kuwa mabingwa wa mashindano ya Dance 100% 2015 baada ya kujivunia alama za kutosha na kujinyakulia zawadi ya ushindi shilingi milioni 5 sambamba na kombe kama ishara ya taji hilo, wakifuatiwa na Team Ya Shamba walioshika nafasi ya pili na kujinyakulia shilingi milioni 1 wakifuatiwa na Best Boys Kaka Zao waliokamata nafasi ya 3 na zawadi ya shilingi laki 5.

Wakiongea baada ya kushinda taji hilo, The WD wameeleza kuwa wanafurahi sana kwa kuweza kubeba heshima hiyo kubwa, kuweza kupenya kutoka mchujo wa makundi shiriki yapatayo 50 yaliyoweza kujitokeza kwa mwaka huu, sambamba na kutoa shukrani kwa East Africa Radio na East Africa Television kwa kuwapatia jukwaa la kuonesha uwezo wao.
Mashindano hayo yalifanyika kwa raundi mbili, ya kwanza ikihusisha makundi kucheza muziki - megamix ambazo walitengeneza wenyewe zikibeba asilimia 40% ya jumla ya alama, huku mzunguko wa pili ukihusisha makundi hayo kucheza muziki walioandaliwa na kubeba alama 60%.

Makundi ya The Winners Crew waliokuwa wanawania taji hilo kwa mwaka wa tatu sasa na Team Makorokocho ambao ilikuwa ni mara ya kwanza kushiriki wanabaki katika rekodi kama washiriki walioweza kupambana kuingia katika fainali za mashindano hayo kwa mwaka huu.

Usikose kutazama eNewz kesho kujionea kwa undani matukio muhimu yaliyojiri katika fainali hizo mpaka kupatikana kwa mshindi na kumbuka, Dance 100% 2015 inadhaminiwa na Vodacom Tanzania na Cocacola, kinywaji rasmi cha Dance 100% 2015.

HABARI ZAIDI

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe