Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Sikumuita Chid Benz, alijileta - JUX

Jumanne , 16th Oct , 2018

Msanii wa muziki wa Bongofleva, Juma Mussa maarufu 'Jux' hatimaye amefunguka kuhusiana na madai ya kutomlipa msanii wa HipHop, Chidbenz baada ya kutumbuiza katika 'show' ya 'In Love & Money' iliyoandaliwa na yeye mwenyewe Jux pamoja na Vanessa Mdee.

Akipiga stori na www.eatv.tv, Jux amesema Chid Benz hakuwa kwenye listi ya wasanii wanaotumbuiza katika tamasha hilo, zaidi alimfuata 'backstage'(nyuma ya jukwaa) wakati 'show' ikiendelea na kumuomba kutumbuiza, hivyo hafahamu madai anayoyatangaza yametokana na makubaliano gani.

Kwanza kabisa Chid hanidai pesa yoyote kwasababu ile 'show' tulivyofika Dar tulikua tayari tumepanga wasanii watakaotumbuiza, hatukuwa na mdhamini, hata wale wasanii baadhi yao kuna vitu tulikua tunawafanyia lakini hatukuwalipa hela, wengi walikuja kutusapoti kama wasanii wenzetu”, amesema Jux.

Chid alinifuata 'backstage' na akasema braza naweza kufanya kitu kwa mashabiki, nikamuheshimu kama braza wangu na msanii mkubwa katika tasnia yetu, akapanda stejini, asubuhi ananipigia ananiambia braza mimi nimefanya 'show' lakini sijapata chochote nikamwambia ok! nitakupa chochote kama asante, ila haikuwa katika maelewano yetu kiasi kwamba anaenda kulalamika kwenye vyombo vya habari kwamba ananidai”, ameongeza.

Kuhusiana na hali ya msanii Chid Benz ilivyo kwasasa, Jux amesema anasikitishwa kumuona msanii huyo akitumiwa katika mambo maovu ambayo hayawezi kumjenga kimaendeleo badala yake imekuwa ni utani unaoendelea kuwafurahisha mashabiki.

Mimi nasikitika kumuona Chid alivyo, naomba tumtumie kumuendeleza na kumjenga, nikipata muda nitamtafuta kama ni pesa nitampatia ila sio kwaajili ya 'show' sikumuita na sikupanga

Msanii Jux anajipanga kuja na album yake mpya kwa mara ya kwanza, itakayoenda kwa jina la 'IN LOVE' anayopanga kuiachia mwakani.
 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa