Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Hatutoi mikopo kwa kuangalia jina la chuo - Wizara

Alhamisi , 1st Dec , 2016

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Mhandisi Stella Manyanya amesema kuwa serikali haitoi mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu kwa kuangalia jina la chuo au ubaguzi wa wanafunzi.

Mhandisi Stella Manyanya akiwa Kikaangoni

 

Ametoa kauli hiyo katika ofis za EATV wakati akijibu maswali ya wananchi kupitia kipindi cha KIKAANGONI kinachoruka kila Jumatano kupitia ukurasa wa Facebook wa EATV.

Alilazimika kutoa kauli hiyo kutokana na malalamiko kutoka kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kampala tawi la dar es Salaam walioandamana hadi ofisi za wizara hiyo wakilalamika kukosa mikopo kwa madai kuwa mikopo hiyo inatoka kwa ubaguzi wa kivyuo.

Naibu Waziri huyo amesema kuwa wanafunzi hao wanapaswa kufuata taratibu za kufahamu ni jinsi gani mikopo hiyo inavyotolewa na wafuate utaratibu wa kutoa malalamiko na serikali itaweza kuyachukulia kama changamoto na kuyatatua.

 

Kuhusu madai ya wanafunzi hao, Manyanya amesema amewasikiliza na kubaini kuwa kuna baadhi yao wana hoja za msingi ikiwemo kuwa na vigezo kama vile uyatima na kozi za vipaumbele, lakini akawataka watafute viambatanisho vya ushahidi wa vigezo vyao, na kisha wafuate taratibu za kukata rufaa kupitia Bodi ya Mikopo.

Katika hatua nyingine Mhandisi Manyanya amewataka viongozi wa vyuo mbalimbali wasikilize kero za wanafunzi wanaowaongoza na kuzipeleka sehemu husika na siyo kufanya mgomo na maandamano jambo ambalo haliwezi kusaidia katika utatuzi wa kero zao.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava