Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

 Afukuzwa kazi kisa kummwagia maji ombaomba

Jumanne , 2nd Oct , 2018

Mfanyakazi wa mgahawa mmoja katika mji wa New York nchini Marekani amefukuzwa kazi kufuatia video iliyosambaa mtandaoni iliyomuonesha  akimmwagia maji raia mmoja asiye na makazi aliyekuja katika mgahawa huo.

Raia huyo aliyejulikana kwa jina la Jeremy Young alikuja katika mgahawa huo unaouza vyakula vya ngano na kahawa kwaajili ya kuchaji simu yake ili aweze kuzungumza na mama yake ndipo alipopitiwa na usingizi.

Baada ya muda kupita ndipo mfanyakazi huyo alipokuja na kummwagia maji akimtuhumu kwa kuwasumbua wateja wake wanaokuja kila siku kupata mahitaji  muda huo huku ajikijichukua video ambayo imesambaa mtandaoni.

Tukio hilo likawalazimisha wamiliki wa mgahawa kutoa taarifa rasmi ya kumfuta kazi na kuahidi kumuomba radhi muathirika wa tukio hilo.

" Mfanyakazi aliyejihusisha na tukio hili ameshafukuzwa kazi na tunafanya jitihada za kumpata muathirika wa tukio ili tuweze kumuomba msamaha ", imesema taarifa hiyo.

" Ninamshangaa mfanyakazi huyu alikuwa na sababu gani ya kufanya tukio hili, kijana wangu ni mkarimu, mpole, hamsumbui mtu na haongei na mtu hadi atakapoongeleshwa ", amesema Betty Jo Craven ambaye  shangazi wa Young.

Jitihada za kumchangia kijana huyo kupitia mtandao zimeweza kuzaa matunda kwa kifikisha kiasi cha dola 7,700 ambazo ni sawa na Shilingi 17.5 millioni za kitanzania.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto