Basil Enatu.
Akiongea na Daily Monitor, mzee Enatu anasema huwa ni raha sana kufanya kazi na maiti kwani hawasumbui na wamekuwa marafiki wakubwa kwake.
“Napenda kufanya kazi na waliofariki kwani maiti hawasumbui kabisa tofauti na watu walio hai”, amesema Enatu.
Enatu ajira yake ni kuwaosha na kuwavisha maiti na wakati mwingine madaktari pia humtaka awasaidie kuvikata vipande vya mwili wakati wa upasuaji wakati mwili unafanyiwa uchunguzi.
Mzee Enatu baba wa watoto kumi na wawili licha kuipenda kazi yake amesema ina changamoto kwani wengi hukataa hata kumsalimia wakihofia mikono yake.