Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

EXCLUSIVE : Mama aliyepofuka akifuatilia mirathi

Jumanne , 24th Sep , 2019

Mkazi wa Kawe kwa Mzimuni Jijini Dar es Salaam, Bi. Mariam Augustino amepoteza uwezo wake wa kuona kwa muda wa miaka mitatu, ikiwa ni katika harakati za kupigania mirathi ya marehemu mume wake.

Bi Mariam amesema kuwa migogoro ya kifamilia imezuka mara baada ya mumewe kufariki takribani miaka mitatu iliyopita, ambayo imepelekea kupata presha ya macho anayopambana nayo hadi sasa akiwa haoni.

Akizungumza na EATV & EA Radio Digital, Bi Mariam ameeleza jinsi ndugu wa upande wa marehemu mume wake wanavyosababisha usumbufu dhidi yake mara kwa mara, wakimtaka asijihusishe na chochote kinachohusiana na nyumba hiyo licha ya yeye kuwa na hati zote  zinazothibitisha uhalali wa kumiliki na kulipia kodi ya ardhi na jengo mara zote zinapohitajika.

''Familia haikunitendea haki, mimi nilitafuta mali na mume wangu nikatengeneza lakini walijaribu kunipeleka mahakamani na kesi nikashinda. Pamoja na kushinda kesi familia ikaja juu kudai kwamba mali za kwao, kila ninapojitahidi msaada sipati wao wapo wengi na mimi nipo peke yangu", amesema Bi Mariam.

Nae kwa upande wake Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mzimuni Kawe, Hassan Ngonyani ameeleza kwamba mgogogoro uliopo baina ya pande hizo mbili ni wa kimaslahi, ambapo upande mmoja wa familia una umiliki halali wa kiwanja na upande mwingine una umiliki halali wa nyumba.

''Wadogo zake marehemu na wanafamilia wanamwambia kama anataka nyumba yake aitoe katika kiwanja hicho lakini wamekiri kuwa mchango mkubwa wa kujenga nyumba hiyo ulitoka kwa ndugu yao lakini kwa makubaliano ya baba yake ambaye pia ndiye baba yao wao '', ameeleza Hassan Ngonyani.

Aidha Bi.Mariam ameomba msaada kwa Watanzania kufuatilia suala hilo kwani mtu anayemtegemea hivi sasa ni mmoja tu ambaye ni mtoto wake wa kwanza.

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu