Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Jiandae kupokea matangazo kwenye simu yako 2020

Ijumaa , 13th Sep , 2019

Tarajia kuanza kuona matangazo katika App ya WhatsApp, kuanzia mwaka 2020 katika sehemu ambayo 'Status' huwa zinaonekana.

Tangu mwaka 2018, wamiliki wa WhatsApp kampuni ya Facebook, walitangaza kuja na mabadiliko kadhaa mojawapo lilikuwa kuhusu matangazo.

Taarifa iliyopo kwa sasa ni Facebook wameanza kukifanyia majaribio rasmi kipengele hicho kipya katika nchi kadhaa ambazo zina watumiaji wengi wa WhatsApp kama India, Brazil, Marekani na nyinginezo.

Kinachofanyika, baadhi ya watumiaji hupewa uwezo wa kuona matangazo au kama unatumia App ya WhatsApp 'Beta' ambayo ni maalum kwaajili ya kuruhusu majaribio mapya kabla hayajawafikia wengi katika App rasmi.

Baada ya hapo watu hutoa maoni kwa mabadiliko ambayo wanayaona hivyo huwapa urahisi wamiliki kuweza kujua madhaifu na kipi waboreshe kabla hawajaifanya kuwa rasmi au waamue kuachana nayo.

Mpaka sasa WhatsApp ina watumiaji zaidi ya Milioni 340 duniani, tangu Facebook wainunue mwaka 2014 kwa Dola Bilioni 19 katika makubaliano ambayo yaliwekwa mwanzo, inaelezwa mpango wa kuja kuweka matangazo katika WhatsApp haukuwepo na pia waanzilishi wake walipinga hilo lakini kinachoendelea kwa sasa Facebook wameonesha kukiuka.

Mapema mwaka huu mmoja ya waanzilishi wa WhatsApp Jan Koum, alitangaza kuondoka Facebook akiituhumu kukiuka makubaliano na zaidi udhaifu ulionekana katika mfumo wa ulinzi na kulinda faragha za watumiaji kutokana na skendo iliyowakumba Facebook.

HABARI ZAIDI

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji