Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kijiji chenye mila za ajabu

Ijumaa , 29th Mar , 2019

Kijiji cha Mafi Dove kilichopo kusini mwa nchi ya Ghana, chenye wakazi takribani 5000, lakini hakuna kati yao aliyezaliwa kijijini hapo kutokana na mila inayokataza kuzaliwa watoto.

Kama ilivyo kwa vijiji vingi kuwa na tamaduni zao, kijiji cha Mafi Dove kimekuwa na mila hii ambayo imegeuka kuwa mwiba kwa wanawake, kwani wanapokuwa wajawazito na kutaka kujifungua, hulazimika kuondoka kijijini hapo na kwenda kijiji cha jirani, ili aweze kujifungua mtoto wake na kisha kurudi.

Mwananchi wa kijiji cha Mafi Dove asimulia 

 

“Wakati mababu zetu walipokuja katika ardhi hii, sauti kutoka mbinguni ilisikika ikiwaambia hapa ni mahali patakatifu, hivyo ukitaka kuishi ni lazima ufuate masharti, sheria ya hapa ni hakuna mtu anayeruhusiwa kuzalia hapa”, alisikika moja wa wakazi wa kijiji hicho alipohojiwa na BBC.

Hiyo ni moja tu ya mila za ajabu zinazopatikana kijijini hapo, kwani zipo mila zingine ambazo pia wakazi wake wanazitekeleza mpaka sasa, ikiwepo kutofuga mnyama yeyote au hata ndege wa kufuga, na pia hawaruhusiwi kuchinja mnyama yeyote.

Lingine la kushangaza zaidi katika kijiji hicho ni kwamba hakina kaburi hata moja, kwani pia hawaruhusiwi kuzika wafu, hivyo mtu akifa hulazimika kwenda nje ya kijiji ili kuzika ndugu yake.

Mpaka sasa mila hizo zinaendelea kutekelezwa, huku baadhi ya wanawake wakilalamika kupata shida kubwa hususan juu ya mila ya kutojifungua kijijini hapo, kwani hulazimika kutembea umbali mrefu kwenda kijiji kingine kujifungua.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava