Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Lugha 5 za mahusiano na jinsi zinavyofanya kazi

Alhamisi , 19th Sep , 2019

Binadamu tuko na tabia tofauti tofauti lakini utaratibu ndio unasaidia kutuongoza ili tuishi vizuri, ndio maana tunasoma na kujifunza.

Mahusiano

Hivyo hivyo katika mahusiano, kuna vitu vya muhimu vya kuzingatia ili kuyaishi mahusiano yenye upendo, furaha na maelewano. Mshauri wa masuala ya mahusiano, Isack Chalo amezungumzia juu ya umuhimu wa lugha hizo tano kupitia kipindi cha Dadaz cha EATV.

Chalo amesema lugha hizo hutumika kwenye mahusiano ya kudumu, ya muda mrefu na yenye kuleta matokeo kwa wahusika na kwamba zinaweza kutumika hata kwenye mahusiano tofauti na mapenzi.

"Lugha ya kwanza ambayo imeongelewa na wataalam wa mapenzi ni ile kutambua na kumpongeza mtu anapofanya vizuri, hii ni kumpongeza mtu anapofanya vizuri, anapopendeza, kwa sababu kila mtu ana mazuri na madhaifu yake lakini ni vizuri akisifiwa", amesema.

"Lugha ya pili ni suala la kuwa na muda wa kutosha miongoni mwa wahusika katika mahusiano, mahusiano yanadumishwa kutokana na kuwa na muda wa kutosha kujadiliana kuhusu mipango yenu. Lugha ya tatu inayohitajika ni katika mahusiano ni kutoa zawadi, kwa maana ya kwamba wewe unampa zawadi mpenzi wako na yeye anakupa zawadi", ameongeza.

Mtaalam huyo ameongeza kuwa lugha ya nne ni kuhudumiana na kusaidiana, huku lugha ya tano akiitaja kuwa ni habari za mguso, akimaanisha kuwa wapenzi kugusana kunakoonesha kuwa ni watu wa karibu.

Kupata ufafanuzi mzuri wa lugha hizo tano, fuatilia katika video hapa chini.
 

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu