Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mtanzania aliyecheza na John Stones atikisa dunia

Jumanne , 1st Oct , 2019

Kenna Ngoma linaweza likawa si jina maarufu kwa Watanzani wengi, lakini kwenye soka la Uingereza na klabu ya Manchester City ni jina kubwa ambalo lilikatisha ndoto za kucheza soka na sasa ni mfanyabiashara mkubwa.

Kenna Ngoma wa pili kutoka kulia waliosimama, akiwa kwenye Academy ya Man City alipokuwa na miaka 14.

Kenna Ngoma ni Mtanzania ambaye anaishi jijini Manchester akifanya biashara ya Ice Cream ambazo zimemuweka kwenye ramani ya dunia, baada ya kutajwa kwenye orodha ya watu 16 wanaowania kuibuka kinara kwenye shindano la 'The Apprentice 2019'.

Kenna Ngoma (wa 4 waliosimama juu) akiwa na washiriki wenzake.

Kenna Ngoma ana umri wa miaka 24, ni mmiliki wa kampuni ya  Ice Cream zenye kilevi na aliianzisha mwaka 2018 ambapo mpaka sasa inafanya vizuri.

Kabla ya kuwaza kuwa na kampuni hiyo, akiwa na umri wa miaka 12, Kenna Ngoma alikuwa mchezaji wa mpira wa miguu ambapo alipita kwenye vituo kadhaa vya kukaza vipaji vya soka kama Barnsley Academy ambapo alicheza na mlinzi wa kati wa Man City John Stones.

Kenna Ngoma (wa 4 kutoka kushoto waliochuchumaa) akiwa Barnsley Academy)

Kenna ambaye wazazi wake walihamia Uingereza kutoka Tanzania alipokuwa na miaka mitano, alikuwa akicheza mpira mpaka mwaka 2013, akiwa na umri wa miaka 17,  kwenye Academy ya Man City. Lakini aliumia na maumivu hayo yalikatisha ndoto yake ya kucheza soka na kuamua kufanya shughuli zingine.

Katika shindano hilo ambalo lipo kwenye msimu wake wa 15, litaanza kuruka rasmi kesho Oktoba 2, 2019 ambapo washiriki 16 akiwemo Kenna watakuwa wanashindana kuwania nafasi ya kushinda kufanya biashara ya mfanyabiashara mkubwa Lord Alan Sugar.

Mbele ni Lord Alan Sugar ambaye atashirikiana kibiashara ya mshindi.

Shindano hilo ambalo litakwenda kwa wiki 12, mshindi atakabidhiwa kitita cha £250,000 zaidi ya shilingi Milioni 705,699,714. Pia atamiliki kampuni mpya kwa kugawana asilimia 50 na mfanya biashara Lord Alan Sugar.

Kenna Ngoma
 

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu