Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mume anywa sumu kisa mkewe kugoma kupika ugali

Jumatatu , 18th Feb , 2019

Mwanaume mmoja katika Kaunti ya Kakamega nchini Kenya amenusurika kifo masaa machache baada ya wawili hao kugombana sababu ikiwa ni mkewe kukataa kumpikia ugali.

Ugali

Tukio hilo limedaiwa kutokea Jumapili katika kijiji cha Emukaba kilichopo Kaunti hiyo ya Kakamega, ambapo Inadaiwa kuwa mwanaume huyo alimvamia mkewe na kumjeruhi sehemu mbalimbali kwa kisu na kisha mwenyewe kumeza vitu vilivyosadikika kuwa na sumu hadi alipokutwa na majirani na kupelekwa hospitali.

Baada ya kumjeruhi mkewe, mwanaume huyo alimwosha mkewe kwa maji na kumfunika kwa blanketi ili kuficha tukio alilolifanya, lakini majirani waliotembelea nyumbani kwake walikuta mwili wa mwanamke huyo ukiwa amefichwa ndani.

Mshauri Mkuu wa masuala ya kijamii na kijinsia, Peninah Mukabane ambaye alitembelea kijijini hapo amesema, "Tunashuhudia ugomvi wa watu wengi majumbani kutokana na matumizi ya madawa ya kulevya na kutokuwa na uwezo wa kuzikabili changamoto za kifamilia zinazowakabili".

Naye Mkuu wa Kituo Kikuu cha Polisi (ODCP) wa Kaunti ya Kakamega, Joseph Chebii amesema kuwa, "Mtuhumiwa alijaribu kujiua mwenyewe kwa kumeza vitu vilivyosadikika kuwa na sumu na alikimbizwa hospitali kwa matibabu".

Hata hivyo kwa mujibu wa ODCP Chebii, mwanaume huyo alifariki akiwa hospitalini na mwili wake kupelekwa mochwari, huku akisema polisi inaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava