Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mwanamke asimulia jinsi harusi ilivyompa UKIMWI

Jumamosi , 5th Dec , 2020

Veronica Lyimo ni mkazi wa jiji la Dar es Salaam, ambapo ameitaja siku ya harusi ya rafiki yake kubadili historia ya maisha yake, baada ya kujikuta akishiriki tendo la ndoa na mpenzi wake wa siku nyingi bila kutumia kinga na ndipo alipojikuta amepata maambukizi.

Veronica Lyimo, anayeishi na Virusi vya Ukimwi

Veronica amesimulia hadithi yake hiyo kwenye kipindi cha MamaMia kinachoruka kila siku za jumatatu hadi Ijumaa kupitia East Africa Radio, ambapo ameeleza kuwa mara ya kwanza kupima UKIMWI ilikuwa mwaka 2015, ambapo vipimo vya awali vilikuwa tata na ndipo alipoamua kwenda Hospitali ya Taifa Muhimbili na ndipo alipoambiwa kuwa tayari ni mwathirika wa VVU.

Veronica anasema kuwa mara baada ya kupokea majibu hayo, alimua kumshirikisha mpenzi wake, lakini mpenzi wake huyo majibu hayo hayakumshangaza kwa kuwa yeye alikuwa akifahamu toka awali kuwa anayo maambukizi.

"Nilipomwambia mpenzi wangu hakushtuka kabisa, kumbe yeye mwenzangu alikuwa anaijua hali yake ya awali kuwa alikuwa na maambukizi, baada ya kupata hayo majibu nililazwa wodi ya vichaa kwa miezi mitatu kwa sababu nilipata sonona, baada ya kutoka mjomba wangu akanichukua na kunipa ushauri nasaha na kunikutanisha na club za vijana wanaoishi na maambukizi", amesimulia Veronica.

Tazama video hapa chini

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu