Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wafahamu wapenzi mavampire wanaoishi hadi sasa

Jumatano , 13th Mar , 2019

Neno Vampire sio geni masikioni mwa wengi, hasa wale wafuatiliaji wa filamu mbali mbali hasa za kutisha.

Kwa mujibu wa tafiti mbali mbali zilizofanywa na wataalamu wa masuala ya utafiti kutoka chuo kikuu cha Havard cha Marekani, Vampire ni viumbe ambao mpaka sasa inaaminika ni 'myth' (hadithi za kusadikika) ambao waliwahi kuwepo kwenye karne ya 17, huko barani Ulaya.

Viumbe hawa walisaidikika kuwa moja ya tishio kubwa sana kwa uhai wa watu, kutokana na kunyonya damu za watu na kuzinywa hadi mtu huyo anakufa, au na yeye kubadilika kuwa vampire.

Kama ambavyo bado inaaminiwa ni viumbe wa kusadikika kwa sababu hakukuwa na 'ushahidi mkubwa' wa uwepo wao, lakini hivi sasa dunia nzima ukitaja neno vampire lazima itajulikana ni kiumbe gani anazungumziwa.

Wapenzi vampire

Hili linawezekana likawa la ajabu lakini ukweli ni kuwa huko nchini Uingereza wapenzi wawili wameaminika kuwa na chembechembe za viumbe hawa hatari, kutokana na kuwa na tabia kama zao za kunywa damu za watu.

Ingawa mpaka sasa hakuna tukio la mauaji lililoripotiwa kuwahi kulifanya, lakini wapenzi hawa wanaojulikana kwa majina ya Lia Benninghoff (26) na Aro Draven (44) wamekuwa wakinywa damu zao kama chakula chao ambacho wenyewe wanadai ndio uhai wao.

Lia anasimulia kwamba alikutana na Aro kwenye mtandao wa kijamii na wakapanga kuonana, na alipomwambia kwamba yeye ni vampire akafurahia na kumuomba amgeuze ili wafanane.

“Kuanzia muda tulionana na tu, nilijua yeye ndiye, na aliponiambia kuwa yeye ni vampire nilishangazwa na kufurahi, sikuwahi kuamini kuwa vampire wapo, ingawa nilitumaini sana wapo”, alisema Lia.

“Aliponiambia kushea damu itatufanya tuwe karibu zaidi, nilimuomba anibadilishe, Aro akajikata na kiwembe nyuma ya mkono wake na kunipa damu, kisha nikajikata nami nikampa yangu akanywa, ghafla nikajisikia nguvu ya ajabu ndani yangu, ilinichukua siku nzima kubadilika, ilikuwa ni maajabu lakini ni nzuri zaidi kuliko ngono”, aliendelea kusimulia Lia.

Lia aliendelea kusimulia kuwa anapenda sana maisha hayo na kwa sasa anakunywa hadi mara nne kwa wiki, na asipokunywa hujihisi mdhaifu.

Hata hivyo wapenzi hao huwa wananunua nguruwe kwa ajili ya kupata damu ya kunywa, na pia huwa wanakunywa damu zao wenyewe tu, na sio za watu wengine.

Familia za wawili zimekubaliana na hali zao, baada ya vipingamizi vikubwa kutoka kwa wazazi wa Aro, ambao waliweka wazi kuwa walimuasili mtoto huyo alipokuwa na miaka mitano.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava